Skip to main content

Posts

Showing posts from August 13, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

PROF. MKENDA: VETA ITOE UJUZI UNAOKIDHI MAHITAJI YA SOKO LA AJIRA

 WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amezitaka Kamati za Ushauri wa Stadi (Training Advisory Committees–TACs) za Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kuwa chachu ya kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira na uzalishaji nchini. Prof. Mkenda amesema kamati hizo zinapaswa kuwa kiungo madhubuti kati ya VETA, Serikali, waajiri na sekta binafsi, ili kuhakikisha vijana wanaohitimu wanakuwa na ujuzi, umahiri, ubunifu na uwezo wa kutumia teknolojia unaohitajika katika maeneo ya kazi. Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda Ameyasema hayo leo, Agosti 13, 2026, jijini Dodoma, wakati akizindua rasmi Kamati za Ushauri wa Stadi za VETA, ambapo amesisitiza kuwa mfumo wa mafunzo ya ufundi stadi haupaswi kuishia katika kutoa vyeti pekee, bali unapaswa kuwaandaa wahitimu kwa ajira, kujiajiri na kuanzisha shughuli za uzalishaji. “Hatupaswi kuwa na mfumo wa mafunzo unaoishia katika kutoa vyeti pekee. Tunataka...

MBUNGE SURATI AAMBATANA NA WAZIRI BASHIRU KUFUATILIA MAENDELEO JIMBO LA SERENGETI

 MBUNGE wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Daniel Surati ameambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, katika ziara ya kikazi wilayani Serengeti, iliyolenga kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kusikiliza changamoto za wananchi na kuweka mikakati ya kuboresha huduma muhimu katika jimbo hilo. Katika ziara hiyo, Waziri Dkt. Bashiru amekutana na kufanya kikao na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Serengeti, ambapo masuala mbalimbali ya maendeleo na changamoto zinazowakabili wananchi yalijadiliwa. Ziara hiyo pia ilimfikisha Waziri katika Kata ya Matare, ambako alizindua vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Igina, hatua inayotarajiwa kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa wanafunzi wa shule hiyo. Mbunge Mary amesema kushiriki kwake katika ziara hiyo ni sehemu ya kuendelea kusimamia kwa karibu masuala ya maendeleo ya wananchi wa Serengeti, akieleza kuwa uwepo wa viongozi katika maeneo ya wananchi unasaidia kupata ...

ZIARA YA RAIS SAMIA URUSI YAZIDI KUZAA MATUNDA, WANAFUNZI 10 WAPATA UFADHILI WA KUSOMA MOSCOW

 Ziara Rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nchini Urusi imeendelea kuzaa matunda katika sekta ya elimu, baada ya wanafunzi 10 waliofanya vizuri katika masomo ya sayansi kupata ufadhili wa masomo katika Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN University) kilichopo jijini Moscow. Wanafunzi hao waliomaliza kidato cha sita na kufanya vizuri katika tahasusi za PCM, PGM na PMC, wamepata fursa hiyo kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended, ikiwa ni sehemu ya matokeo ya ziara ya Rais Samia nchini Urusi iliyofanyika mwezi Juni 2026. Rais Samia alifanya ziara hiyo nchini Urusi na kutunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) na RUDN University, moja ya vyuo vikuu vinavyotambulika nchini humo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Agosti 13, 2026, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesema wanafunzi hao wamechaguliwa kutokana na kufanya vizuri kitaaluma, wakifuata kundi ...

PROF. MKENDA: VETA ITOE UJUZI UNAOKIDHI MAHITAJI YA SOKO LA AJIRA

 WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amezitaka Kamati za Ushauri wa Stadi (Training Advisory Committees–TACs) za Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kuwa chachu ya kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira na uzalishaji nchini. Prof. Mkenda amesema kamati hizo zinapaswa kuwa kiungo madhubuti kati ya VETA, Serikali, waajiri na sekta binafsi, ili kuhakikisha vijana wanaohitimu wanakuwa na ujuzi, umahiri, ubunifu na uwezo wa kutumia teknolojia unaohitajika katika maeneo ya kazi. Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda Ameyasema hayo leo, Agosti 13, 2026, jijini Dodoma, wakati akizindua rasmi Kamati za Ushauri wa Stadi za VETA, ambapo amesisitiza kuwa mfumo wa mafunzo ya ufundi stadi haupaswi kuishia katika kutoa vyeti pekee, bali unapaswa kuwaandaa wahitimu kwa ajira, kujiajiri na kuanzisha shughuli za uzalishaji. “Hatupaswi kuwa na mfumo wa mafunzo unaoishia katika kutoa vyeti pekee. Tunataka...

UGANDA KUHAMISHA WIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI KUTOKA KAMPALA

  KAMPALA, Uganda   Serikali ya Uganda imepanga kuanza kuhamisha kwa awamu wizara, idara na taasisi zake kutoka Kampala kwenda Nakasongola , katika mpango wa muda mrefu ambao unaweza kuendelea hadi mwaka 2040 . Mpango huo umetangazwa na Waziri wa Nchi wa Maendeleo ya Miji, Margaret Muhanga , mbele ya Kamati ya Ardhi na Nyumba ya Bunge la Uganda. Muhanga amesema Rais Yoweri Museveni anaunga mkono mpango huo, ambao Serikali inautazama kama sehemu ya utekelezaji wa maono ya maendeleo ya Uganda kuelekea mwaka 2040. KAMPALA YAWA CHANGAMOTO Serikali imesema msongamano mkubwa wa magari na changamoto za upangaji wa mji zimefanya Kampala kuwa na mazingira magumu kwa watu kuishi na kufanya kazi. Muhanga amesema Uganda inapoteza takribani dola bilioni 1.6 kwa mwaka kutokana na foleni za magari, huku baadhi ya wakazi wakilazimika kuamka saa 10 alfajiri (4:00 asubuhi) ili waweze kufika kazini saa 2 asubuhi (8:00) . “Kampala haiwezi kuishiwa, haiwezi kubadilishwa, haiwezi kuendelez...

MBUNGE NSEKELA AHAIDI KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI KIMULI

   Na Angela Sebastian ;Kyerwa Mbunge wa Kyerwa, Khalid Nsekela, ameahidi kushirikiana na Halmashauri pamoja na wadau wa elimu kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika Shule ya Sekondari Kimuli, ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda mwingi kujisomea badala ya kutembea hadi saa nne kufuata maji. Ahadi hiyo imekuja wakati wa afla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha sita 2026, licha ya shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, ambapo katika matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2026 ilishika nafasi ya kwanza wilayani,ya kwanza kwa shule za Serikali kimkoa na ya pili kimkoa kwa shule zote. Kimuli inakabiliwa pia na changamoto ya ukosefu wa ofisi za walimu na mabweni, hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi kulala katika vyumba vya madarasa visivyo na madirisha lakini wanafanya vizuri katika masomo yao. Kwa niaba ya Mbunge, Nekmia Nguma Katibu wa Mbunge-Kitengo cha Mahusiano, amesema Nsekela amewapongeza wanafunzi na...

MBUNGE NSEKELA AHAIDI KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI KIMULI

 Na Angela Sebastian ;Kyerwa Mbunge wa Kyerwa, Khalid Nsekela, ameahidi kushirikiana na Halmashauri pamoja na wadau wa elimu kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika Shule ya Sekondari Kimuli, ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda mwingi kujisomea badala ya kutembea hadi saa nne kufuata maji. Ahadi hiyo imekuja wakati wa afla ya utoaji tuzo kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha sita 2026, licha ya shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, ambapo katika matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2026 ilishika nafasi ya kwanza wilayani,ya kwanza kwa shule za Serikali kimkoa na ya pili kimkoa kwa shule zote. Kimuli inakabiliwa pia na changamoto ya ukosefu wa ofisi za walimu na mabweni, hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi kulala katika vyumba vya madarasa visivyo na madirisha lakini wanafanya vizuri katika masomo yao. Kwa niaba ya Mbunge, Nekmia Nguma Katibu wa Mbunge-Kitengo cha Mahusiano, amesema Nsekela amewapongeza wanafun...

NAIBU WAZIRI MAKAMBA AITAKA PBPA KUENDELEA KUTOA ELIMU KWA UMMA

 Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb.), ameitaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili wananchi wawe na uelewa mpana kuhusu majukumu ya Wakala na mchango wake katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini. Mhe. Makamba ametoa wito huo alipotembelea banda la PBPA katika maonesho yanayofanyika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya Tamasha la Kizimkazi 2026. Amesema ni muhimu wananchi wakaendelea kuelimishwa kuhusu Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja na namna PBPA inavyotekeleza majukumu yake katika kusimamia uagizaji wa bidhaa za mafuta kwa lengo la kuhakikisha nchi inakuwa na uhakika wa upatikanaji wa bidhaa hiyo muhimu. Aidha, Mhe. Makamba ameipongeza PBPA kwa utendaji wake katika kutekeleza majukumu yake na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, amemweleza Naibu Waziri kuwa Wakala unaendelea kutekeleza majuk...