_Kiwanda cha Shengde chakaribia kuanza uzalishaji rasmi mwezi Julai_ *Juni 26, 2025- Dodoma* Mkoa wa Dodoma unajiandaa kuandika historia mpya katika sekta ya usafishaji wa madini, kufuatia hatua za mwisho za ujenzi wa kiwanda kipya cha Shengde Precious Metal Resources Company Ltd, kilichopo eneo la Nala, ambacho kinatarajiwa kuanza rasmi uzalishaji wa copper cathode mwezi Julai, 2025. Katika ziara maalum ya ukaguzi, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Menard Msengi, amesema ujenzi wa kiwanda hicho ni hatua kubwa kuelekea utekelezaji wa agizo la Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde, la kuhakikisha kuwa hadi kufikia Julai 30, 2025, usafishaji wa shaba yote inayochimbwa nchini unafanyika ndani ya mipaka ya Tanzania. “Ujio wa kiwanda hiki ni kichocheo muhimu katika maendeleo ya Sekta ya Madini mkoani Dodoma na nchini kwa ujumla,” amesema Mhandisi Msengi, na kuongeza kuwa, “mradi huu utawanufaisha wachimbaji wadogo kwa kuwapatia soko la uhakika, kuongeza thamani ya madini...
Marato tv - Sauti ya Jamii