Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga Elimu ni gharama. Elimu ina mahitaji mengi ambayo yanahitaji fedha ili kuyakamilisha ili kupata utulivu wa kujifunza darasani. Serikali inasimamia na kutekeleza kikamilifu Sera ya Elimumsingi Bila Ada ambapo hutumia fedha nyingi kuwezesha upatikanaji wa mahitaji muhimu shuleni ili shughuli za ufundishaji na ujifunzaji ziweze kufanyika vizuri na kuwapunguzia mzigo wazazi na walezi gharama za kusomesha watoto wao. Kupitia Sera ya Elimumsingi Bila Ada, fedha zinawafikia walengwa ipasavyo. Serikali hutuma fedha moja kwa moja katika akaunti za benki za shule ili zigharimie masuala mbalimbali ya kuendesha shule kama vile shughuli za utawala, taaluma, mitihani, ukarabati, michezo na mahitaji mengine kadha wa kadha. Sambamba na hilo, serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inatoa ufadhili kwa wanafunzi wanaosoma Stashahada kwa kozi za kipaumbele, Shahada ya kwanza na kuendelea katika kozi mbalimbali ili kwa pamoja vijana wa Kitanzan...
Marato tv - Sauti ya Jamii