▪️Waziri Mavunde na Waziri Kabamba wakubaliana msingi wa ushirikiano, ▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia na Rais Tshisekedi ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili, ▪️Ushirikiano walenga kurahisisha usafirishaji na biashara ya madini, ▪️Wakubaliana kuweka mikakati ya pamoja kuimarisha ufuatiliaji wa uzalishaji wa madini (traceability), *TIANJIN, CHINA* Pembezoni mwa Mkutano wa Madini wa China uliofanyika Jijini Tianjin, Waziri wa Madini *Mhe. Anthony Mavunde* amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), *Mheshimiwa Louis Watum Kabamba* yaliyolenga kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano kwenye sekta ya madini. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika tarehe 11 Septemba, 2026 Waziri Mavunde na mwenzake Mhe. Kabamba walijadiliana kwa kina namna ya kuendeleza sekta ya madini baina ya Nchi zao na hatimaye kuweka msingi ambao utakuwa ni mwanzo wa kuimarisha ushirikiano utakaoleta tija kwa pande zote mbili. "Leo tumekutana hapa si kwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii