Mhe Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara na Mkurugenzi wa taasisi ya Matiko Foundation ameendelea na ziara yake ndani ya Wilaya ya Tarime kwa kuzitembelea Shule za Sekondari Nkende na Rebu zinazopatikana ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime na kufanya mazungumzo na Walimu na Wanafunzi wa Shule hizo. Ikiwa ni utendaji wa majukumu yake ya kibunge, Mhe Esther Matiko amezungumza na Walimu hao na kupokea changamoto mbalimbali ambazo atakwenda kuziwasilisha bungeni kwa ajili ya kufanyiwa kazi na serikali kuu. Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkende Mwl Nchagwa Chacha amemueleza Mhe Esther Matiko changamoto kubwa inayoikabili Shule hiyo ni ukosefu wa Mabweni ya Wanafunzi, jambo lililopelekea Shule hiyo kuanzisha mchakato wa ujenzi kwa kushirikiana na wazazi na wadau wengine wa elimu. Sambamba na changamoto hiyo Mwl Chacha hakusita kumpongeza Mhe Esther Matiko kwa kutimiza ahadi zake alizoahidi shuleni hapo ikiwa ni pamoja na utoaji wa Taulo za Kike kupitia taasisi ya Matiko...
Marato tv - Sauti ya Jamii