Kuelekea fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, washiriki wa fani ya upishi katika Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi WorldSkills Tanzania 2026 wametakiwa kujiandaa kuwa mabalozi wa utalii na ukarimu wa Tanzania kupitia umahiri wao wa kupika. Wito huo umetolewa leo Agosti 22,2026 na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Bi. Bernadetta Ndunguru, alipotembelea mashindano yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga. Ndunguru amesema washiriki hao tayari wameonesha kiwango cha juu cha taaluma na wanapaswa kujiona kama wapishi wakubwa watakaokuwa sehemu ya kuipokea Afrika wakati Tanzania itakapokuwa mwenyeji wa AFCON 2027. Kwa mujibu wa Ndunguru, ubora wa huduma za chakula na ukarimu vinatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya taswira ya Tanzania mbele ya maelfu ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika. "Niwahimize vijana muendelee kuboresha ujuzi wenu na kutumia fursa ya WorldSkil...
Marato tv - Sauti ya Jamii