_▪️Asema Rais Dkt. Samia amewapa urithi watoto wa kitanzania wa kupata elimu_ _▪️Apongeza utekelezaji wa mradi huo kwa viwango_ Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameweka jiwe la msingi la uzinduzi wa shule ya Sekondari ya Mbatakero iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ambayo imejengwa kupitia mradi wa SEQUIP Ujenzi wa Shule hiyo ambao umegharimu shilingi milioni 584 itasaidia kuondoa adha wanayopata wanafunzi wa eneo hilo ya kutembea umbali mrefu wa kwenda shule za jirani za sekondari za Roo na Longoi ambazo ziko umbali wa kilometa 9 kwa kila shule kutoka Kijiji cha Mbatakero na Pia itasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule hizo. Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ujenzi wa shule hiyo ni matokeo ya maamuzi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha anaondoa changamoto kwa wananchi “Kama mlivyosikia, Rais Dkt. Samia anapoelezewa kuna shida, anasema viongozi watatue changamoto...
Marato tv - Sauti ya Jamii