📍Wafanyabiashara wakiri kumalizika kwa uhasama wa 'Paka na Chui', taasisi za fedha zaahidi ushirikiano NA Mashaka Mhando, Tanga MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, ambapo makusanyo ya kodi yamepanda kutoka Shilingi Bilioni 531 mwaka 1996/1997 hadi kufikia Shilingi Trilioni 32 kwa mwaka uliopita. Hayo yamebainishwa leo wakati wa matembezi maalum ya hisani na mazoezi yaliyoanzia katika ofisi za TRA Mkoa wa Tanga hadi viwanja vya Usagara, yakiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 30 ya mamlaka hiyo na maandalizi ya Tuzo ya Rais kwa Mlipakodi Bora. Akizungumza baada ya kuongoza matembezi hayo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, aliipongeza TRA kwa hatua kubwa iliyopigwa na kueleza kuwa Mkoa wa Tanga umefanya vizuri kwa kuvuka malengo ya makusanyo kwa asilimia 100. Balozi Batilda alieleza kuwa kukua kwa shughuli za Bandari ya Tanga, mipaka ya Horohoro, na wilayani kumeufan...
Marato tv - Sauti ya Jamii