Na Elizabeth Zaya BAADHI ya wakazi wa Songea mkoani Ruvuma wamefurahia ujio wa Tamasha la Kitaifa la utamaduni mkoni Ruvuma kwa kuwapa fursa za kufanyabiashara na kujitangaza kupitia tamasha hilo. Kadhalika, wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha utaratibu huo wa kuwa na tamasha la utamaduni kwa kuwa pamoja na kuwakumbusha kuenzi tamaduni zao lakini wanalitumia kujinufaisha kiuchumi. Tamasha la Utamaduni la Kitaifa linatarajiwa kufanyika kwa mara ya tatu mkoani Ruvuma kuanzia Septemba 20 mpaka 23 na mgeni rasmi kwenye kilele chake ni Rais Samia. Tito Mbilinyi, mkazi wa Songea mkoani Ruvuma, anasema matamanio yao kwa miaka mingi ilikuwa kuona tamaduni zao zinaendelezwa, hivyo wanampongeza Rais Samia kwa kuliona hilo na kuruhusu kufanyika. “Mimi namshukuru sana Rais Samia kwa kutuletea tamasha hili, tulilisubiri sana, kwa hiyo tumefarijika sana,"anasema Mbilinyi. Sisi kama wafanyabiashara tunasema hivi, karibu mgeni, mwenyeji apone, kwa sababu hata mwenye nyumba ya ku...
Marato tv - Sauti ya Jamii