Wananchi wa Jimbo la Serengema Mkoani Mwanza wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Sengerema Hamis Tabasam kwa kufanikisha ujenzi wa shule 24 za sekondari kwa kipindi cha miaka minne ambapo awali kulikuwa na sekondari sita tu kipindi cha mbunge aliyemaliza muda wake wa miaka 15 akiwa katika jimbo hilo. Mbunge wa Jimbo la Sengerema mkoani Mwanza Hamis Tabasam kwa kushirikiana na wananchi wamefanikiwa kukamilisha ujenzi wa shule za sekondari mpya tatu katika eneo la Igalagalilo, Chamabanda na Kasomeko ili kunusuru wanafunzi kutembelea umbali wa kilometa 16 kwenda shule za jirani.
Marato tv - Sauti ya Jamii