Skip to main content

Posts

Showing posts from May 4, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mjumbe wa Kamati Kuu Ccm, Leila Ngozi Awasili Bariadi Kusimamia Uwasilishaji Wa Ilani ya Chama – “ccm Inatenda, na inaeleza, "

BARIADI, SIMIYU  Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Mlezi wa Mkoa wa Pwani, Leila Ngozi, amewasili rasmi katika Jimbo la Bariadi kwa ziara maalum ya kusimamia na kushuhudia uwasilishaji wa Ilani ya CCM 2020–2025, hatua inayolenga kuimarisha uwajibikaji wa viongozi na kuonesha utekelezaji wa ahadi kwa wananchi. Katika ziara hiyo, Mhandisi Kundo Mathew, Mbunge wa Jimbo la Bariadi, amepewa jukumu la kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani hiyo mbele ya Mjumbe huyo wa Kamati Kuu, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Bariadi, na viongozi mbalimbali wa chama na serikali. > “Leo Bariadi tunajivunia kupata heshima ya kupokea kiongozi wa juu wa Chama – Mjumbe wa Kamati Kuu. Huu ni uthibitisho kuwa CCM haiteleki maeneo yake – na kila ahadi iliyotolewa kwa wananchi ni agizo linalopimwa kwa vitendo,” alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo. Tukio hilo limeambatana na mapokezi makubwa na msisimko wa kisiasa, ambapo viongozi wa mashina, kata, tarafa na wilaya w...

Wakigawa Jimbo Nitagombea Bariadi Vijijini-Eng Kundo

BARIADI, Simiyu  Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhandisi Kundo Mathew, ametangaza kuwa endapo Jimbo hilo litagawanywa rasmi, atagombea tena Ubunge kupitia Jimbo la Bariadi Vijijini – eneo analotokea na analosema lina uhitaji mkubwa wa maendeleo ya karibu. Akizungumza leo katika Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Bariadi uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Bariadi Alliance, Mhandisi Kundo aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020–2025 mbele ya wajumbe wa mkutano huo, huku akitumia jukwaa hilo kueleza dhamira yake ya kuendelea kulitumikia Taifa kupitia mzizi wake wa kijijini. > "Kuna mkakati wa kugawa Jimbo la Bariadi kutokana na ukubwa wake wa kata 31. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imefika kukusanya maoni na sisi kama viongozi tumeonyesha nia njema ya kupendekeza mgawanyo huo ili kurahisisha shughuli za maendeleo na kuwasogezea wananchi huduma muhimu," alisema Mhandisi Kundo. Aidha, alieleza wazi kuwa iwapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania a...

Nmb Yakabidhi Vifaa Vya Milioni.42.4 Kigoma,Wadau Wahimizwa Kuunga Mkono Serikali

OR-  TAMISEMI Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI Mhe. Zainabu Katimba  amepokea Vifaa vyenye thamani ya shilingi Mil.42.4 kwa ajili ya huduma za Afya na Elimu kutoka Benki ya NMB ikiwa ni sehemu ya benki hiyo kurejesha kwa Jamii. Akipokea vifaa hivyo Mhe. Katimba amesema serikali inaendelea kuhakikisha inapeleka maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Afya,Elimu na miundombinu hiivyo amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali ili kuwaletea maendeleo wananchi.  “Tuwashukuru sana wadau wetu wakubwa wa NMB tunatambua jitihada zenu za kuunga mkono serikali kwa juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita katika sekta nyingi ikiwemo Afya na Elimu” amesema Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa na Kaimu meneja wa NMB kanda ya Magharibi Gardiel Sawe ni vifaa vya kujifungulia, Viti  vitano (05) kwa ajili ya Wagonjwa, Vitanda kumi (10) kwa ajili ya Wajawazito kujifungulia  ambavyo vyote vimetole...

Kisanga Rais Ruto akirushiwa Kiatu Mkutanoni Migori

  ZIARA ya Rais William Ruto katika Kaunti ya Migori Jumapili ilikumbwa na kisanga baada ya kiongozi wa nchi kupigwa na kiatu alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara Kwenye mji wa  Kehancha Ulioko eneo Bunge la  Kuria Magharibi . Kiatu kilionekana kikirushwa kutoka kwa umati na kumpiga Rais Ruto akiwa katikati ya hotuba yake. T ukio hilo lilitokea wakati Kiongozi wa Taifa alipokuwa ziarani Migori kuzindua miradi ya serikali. Anatarajiwa kuwa katika eneo hilo kwa siku mbili hadi tatu. Dkt Ruto awali alitembelea Suna Mashariki ambako alihudhuria ibada ya maombi ya madhehebu mbalimbali. Baadaye alielekea Suna Magharibi na kuzindua ujenzi wa Chuo cha Kiufundi cha Piny Oyie kabla ya kufungua rasmi ofisi za kaunti ndogo. Matukio yote haya yalifanyika bila vurugu na Rais aliwahutubia wakazi, akiwaeleza mipango ya serikali. Alipofika Kuria, umati uliokuwa ukimsubiri ulikuwa mgumu kudhibiti. Wakati Dkt Ruto alipokuwa akizungumza, umati ulianza kusonga kuelekea jukwaani. Katika hal...

Zimamoto Yaungana na Mataifa Mengine Kuadhimisha Siku ya Wazimamoto Duniani

 *Na Mwandishi wetu - Dar es Salaam*  Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania Bara, limeungana na Wazimamoto  wote Duniani katika kuadhimisha Siku ya Wazimamoto Duniani ambayo hufanyika Mei 4, kila mwaka. Akizungumza na Waandishi wa habari Mei 04, 2025 jijini Dar es Salaam Naibu Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (DCF) Puyo Nzalayaimisi, ambaye pia ni Msemaji wa Jeshi hilo amesema kuwa siku hii ilianzishwa rasmi mwaka 1999 kufuatia tukio lililotokea nchini Australia ambapo wazimamoto watano walifariki wakijaribu kuzima moto katika msitu uliopo eneo la Linton Jimbo la Victoria. Tukio hili liliamsha hisia kwa Wazimamoto wote Duniani na kuamua kuwakumbuka na kuwaenzi kwa kuweka azimio la kuwakumbuka mashujaa wote waliopoteza maisha wakitekeleza majukumu yao kwa kuanzisha Siku ya Zimamoto Duniani. Aidha, Maadhimisho haya yanatambua mchango Mkubwa wa Maafisa na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika kulinda maisha na mali za wananchi dhidi ya majanga mbalimbali yaki...

Tumedhamiria Kuwainua Kiuchumi Wachimbaji Wadogo-majaliwa

_▪️Asema Rais Dkt. Samia ni alama ya ukuaji wa Sekta ya Madini_ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeamua kuwekeza kwenye sekta ya madini ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata kipato na kujikwamua kiuchumi. Amesema Serikali imenunua mitambo 15 ya kisasa ya uchenjuaji ambayo itasambazwa kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo hivyo ametoa wito kwa wachimbaji hao kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na fursa hiyo. Ameyasema hayo leo Jumapili (Mei 04,2025) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Chingumbwa kitongoji cha Namungo Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi. Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Afisa Madini wa mkoa kuendelea na mpango wa kubaini maeneo yenye madini yatambulike na kisha kutoa leseni kwa wachimbaji wadogo ili waweze kufanya shughuli za uchimbaji.  “Pamoja na hili tumeamua maeneo yote ya madini yaliyochukuliwa leseni na...