📍Asema anaheshimu mchango aliopewa na vijana kwa ajili ya fomu 📍 UVCCM wampa fedha za kuchukua fomu, wamuahidi kumuunga mkono Na Mwandishi Wetu, Muheza NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA awewataka vijana kuwa makini katika upigaji wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuhakikisha wanachagua wagombea wenye kesho nyingi kwa ajili ya kusaidia kuleta maendeleo wilayani Muheza. Akizungumza kwenye Kambi ya vijana iliyofanyika shule ya sekondari Chief Mang'enya, MwanaFA ambaye pia ni mbunge wa Muheza alisema kuelekea upigaji wa kura za maoni ni vizuri vijana wakawaunga mkono wagombea wataoivusha CCM katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba. "Kundi hili kama Kila kitu kitakaa sawa na rehema ya mungu, lina kesho nyingi kuliko jana, linatakiwa kuunga mkono vijana wenzao wenye kesho nyingi kuliko kuunga mkono wenye jana nyingi kuliko kesho chache na wana jana nyingi ambazo hawakujali mambo yetu," alisema. Alisema amefurahi k...
Marato tv - Sauti ya Jamii