Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini na mzazi wa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mwita Waitara, amelipongeza Jeshi hilo kwa kuendelea kuwajenga vijana katika misingi ya uzalendo, nidhamu, uwajibikaji na kujitegemea, akisema mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa katika kuwaandaa vijana kukabiliana na changamoto za maisha. Waitara ameyasema hayo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, Operesheni Linda Amani na vijana waliojitolea, iliyofanyika katika Kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mlandizi, mkoani Pwani, ambapo amesema vijana wanaomaliza mafunzo hayo wanapaswa kutumia ipasavyo maarifa na stadi walizopata ili kujiajiri, kushiriki katika shughuli za maendeleo na kuwa raia wema wenye mchango kwa Taifa. Aidha, Waitara amehimiza matumizi sahihi ya teknolojia ya Akili Bandia (AI) katika kuwaandaa vijana kwa mazingira ya sasa, akisema teknolojia hiyo inaweza kutumika kuwaongezea maarifa na stadi mbalimbali zitakazowasaidia kukabiliana na mahit...
Marato tv - Sauti ya Jamii