Skip to main content

Posts

Showing posts from June 28, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MSIGWA: SERIKALI YA SAMIA YAVUNJA REKODI YA MIRADI YA MAENDELEO, UCHUMI WAENDELEA KUPAA

SERIKALI imesema utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umeendelea kuzaa matunda makubwa, huku uchumi wa taifa ukiimarika, mapato ya ndani yakiongezeka na huduma za kijamii zikiboreshwa kwa kiwango kikubwa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema Serikali imeendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi zake kwa kuwekeza trilioni za fedha katika sekta za kimkakati zikiwemo umeme, maji, afya, elimu, kilimo, reli, barabara, bandari na usafiri wa anga. Msigwa ameema mafanikio hayo yanaonesha wazi kuwa Tanzania inaendelea kujenga uchumi imara unaojitegemea, huku utegemezi wa misaada ya nje ukizidi kupungua kutokana na ongezeko kubwa la ukusanyaji wa mapato ya ndani. Ameeleza kuwa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 yenye thamani ya Shilingi trilioni 62.33 ni bajeti ya kihistoria itakayokuwa msingi wa kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku asilimia 74.2 ya fedha zake ...

WAZIRI MKUU: HATUPASWI KUPUUZIA VIASHIRIA VYA UVUNJIFU WA AMANI

 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania waendelee kuhimizana kuhusu ulinzi wa Taifa na kamwe wasipuuze viashiria vya uvunjifu wa amani. "Tuendelee kuhimizana kuhusu suala la ulinzi wa Taifa letu. Ulinzi wa Taifa letu ni wa kila Mtanzania na amani yetu ni ya kila Mtanzania." "Sasa hivi hatupaswi kupuuzia viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Hatutakiwi kuvipuuza kwa sababu vimetuachia doa," amesema. Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 28, 2026) katika ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye usharika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida.  Harambee hiyo ambayo ni ya nne kufanyika, ililenga kukusanya sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya kuboresha vituo vya huduma za afya, kuimarisha vituo vya huduma za elimu, utumishi na uinjilisti vya Dayosisi hiyo ambavyo vinapaswa kukamilika ifikapo Desemba, mwaka huu. Jumla ya sh. bilioni 1.331 zilikusanywa zikiwa ni fedha taslimu na ...

TRA YAHAMASISHA UPANDAJI MITI JIJINI TANGA

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Leo wamefanikiwa kupanda miti isiopungua 1000 katika shule ya sekondari Ummy Mwalimu iliyopo katika kata ya maweni wilayani na hii ikiwa ni muendelezo wa shughuli za kijamii wanazoshiki katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake. Wakiwa katika zoezi hilo mgeni rasmi Naibu kamishna shughuli za ufundi - Kodi za ndani Ted Frank silkiluwasha amesema TRA pamoja na shughuli ilizonazo lakini pia imekuwa mstari wa mbele katika kushiriki mambo ya kijamii na hii na inadhihisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya Mamlaka ya mapato Tanzania na jamii. Aidha Silkiluwasha pia amesisitiza utunzaji wa miti hiyo kwani Kwa kuilinda itasaidia kuilinda ozone laya,leya inayozuia mionzi ya jua kufika katika uso wa dunia ambayo ni hatari sana Kwa afya ya wanadamu na viumbe vingine vilivyopo. Sambamba na hilo amemtaka Meneja wa TRA mkoa wa Tanga kuendelea kutoa elimu ya Kodi kwani elimu hiyo inapaswa kuwa endelevu na ili kuboresha ha...

ELIMU DODOMA YAINGIA HATUA MPYA KUPITIA ZIARA YA WALIMU KOREA KUSINI

 Na Mwandishi Wetu UJUMBE  wa walimu na viongozi wa elimu kutoka Mkoa wa Dodoma wapatao 40 umeondoka kwenda Korea Kusini kujifunza, namna ya kufundisha, kusimamia shule na kutumia teknolojia katika elimu. Ujumbe huo unatarajiwa kushiriki programu ya mafunzo na ziara ya kielimu ya siku nne kamili nchini Korea Kusini, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa walimu walioonesha utendaji bora na kufanikisha ongezeko la ufaulu wa wanafunzi katika Mkoa wa Dodoma. Mratibu wa safari hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Molle  alisema walimu hao waliondoka juzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, Juni 27, 2026, kuelekea Seoul, Korea Kusini, kupitia Doha, Qatar. Alisema ziara hiyo ya kimasomo itafanyika kwa siku nne, ambapo walimu na viongozi wa elimu wanatarajiwa kushiriki katika mafunzo, kubadilishana uzoefu na kujifunza kuhusu matumizi ya teknolojia, ubunifu, uongozi wa shule na mbinu za kisasa za ufundishaji. Al...