SERIKALI imesema utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umeendelea kuzaa matunda makubwa, huku uchumi wa taifa ukiimarika, mapato ya ndani yakiongezeka na huduma za kijamii zikiboreshwa kwa kiwango kikubwa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema Serikali imeendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi zake kwa kuwekeza trilioni za fedha katika sekta za kimkakati zikiwemo umeme, maji, afya, elimu, kilimo, reli, barabara, bandari na usafiri wa anga. Msigwa ameema mafanikio hayo yanaonesha wazi kuwa Tanzania inaendelea kujenga uchumi imara unaojitegemea, huku utegemezi wa misaada ya nje ukizidi kupungua kutokana na ongezeko kubwa la ukusanyaji wa mapato ya ndani. Ameeleza kuwa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 yenye thamani ya Shilingi trilioni 62.33 ni bajeti ya kihistoria itakayokuwa msingi wa kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku asilimia 74.2 ya fedha zake ...
Marato tv - Sauti ya Jamii