Skip to main content

Posts

Showing posts from February 16, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mawaziri Wakutana Lushoto Kutafuta Suluhu ya Migogoro ya Wananchi Mkoani Tanga

Na OWM - TAMISEMI,  Lushoto Mawaziri saba (7) wa kisekta  wakiwa na mwenyeji wao ambaye ni Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe.  Prof. Riziki Shemdoe  ambaye ni Mbunge wa Lushoto wamekutana wilayani Lushoto kujadili utatuzi wa changamoto na migogoro inayowakabili  wananchi mkoani Tanga ikiwemo ya ardhi, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa katika ziara yake ya kikazi inayoendelea mkoani Tanga. Mwenyekiti wa kikao kazi hicho,  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Asiatu Kijaji ameongoza kikao hicho cha viongozi hao na watalaam wa Wizara za Kisekta ambacho kitawasilisha mapendekezo ya utatuzi wa migogoro na changamoto hizo za wananchi kwa Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kabla ya kuhitimisha ziara yake mkoani Tanga, ili kuiwezesha Serikali kuchukua hatua stahiki. Katika kikao kazi hicho wananchi wenye changamoto mbalimbali wamepata fursa ya kuwasilisha malalamiko yao na kusi...

Kamati na Kliniki Za Kisheria

Na George Marato-Dar Mkuu wa mkoa wa Dar es saalam bw Albert Chalamila,amesema kuna janga kubwa la baadhi ya wananchi wa mkoa huo kutegemea urithi mali za wazazi wao hatua ambayo sasa imesababisha migogoro mingi katika familia huku baadhi ya familia hizo zimekuwa zifanya mipango ya kuwaua wazazi wao ili waweze kurithi mali hizo. Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es saalam ametoa kauli hiyo leo Feb 16 mwaka 2026 katika viwanja vya Mnazi mmoja wakati akizindua kamati za kisheria ngazi ya wilaya na mkoa wa Dar es saalam  pamoja na kiliniki ya kisheria iliyoandaliwa na ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali. Kwa sababu mkuu huyo wa mkoa wa Dar es saalam mbali na kuipongeza ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali kwa kutoa huduma  na kusema kuzinduliwa kamati hizo na kiliniki hiyo ya kisheria itapunguza sehemu kubwa ya migogoro katika mkoa wa Dar es saalam. Akizungumza katika hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Kamati hiyo,Mkuu huyo  wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila,ambaye alikuwa mge...

Mbunge Agnes Marwa Atoa Sadaka Maalum Kuunga Mkono Maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Musoma Mjini Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes Marwa, leo ametoa sadaka maalum kwa viongozi wa dini ya Kiislamu katika Misikiti tofauti ya Musoma Mjini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Sadaka hiyo imelenga kuwasaidia viongozi wa dini pamoja na waumini katika kujiandaa na mwezi huo muhimu wa ibada, unaoheshimiwa na Waislamu duniani kote. Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na buswati, tende, kanzu, balaghashee pamoja na fedha taslimu, ambavyo vimekabidhiwa kwa viongozi kutoka misikiti mbalimbali ya Musoma Mjini. Akizungumza wakati wa tukio hilo, Agnes Marwa alisema kuwa sadaka hiyo ni ishara ya mshikamano, upendo na heshima kwa viongozi wa dini, pamoja na kuthamini mchango wao katika kujenga maadili mema na amani ndani ya jamii. “Nimeona ni muhimu kushiriki na ndugu zetu wa Kiislamu katika maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Huu ni mwezi wa ibada, subira, na kusaidiana, hivyo ni wajibu wetu kama viongozi kuendelea kuwa karibu na ...

Kamati na Kliniki Za Kisheria Yazinduliwa Dar Es Saalam Kwa Kishindo

Na George Marato-Dar Mkuu wa mkoa wa Dar es saalam bw Albert Chalamila,amesema kuna janga kubwa la baadhi ya wananchi wa mkoa huo kutegemea urithi mali za wazazi wao hatua ambayo sasa imesababisha migogoro mingi katika familia huku baadhi ya familia hizo zimekuwa zifanya mipango ya kuwaua wazazi wao ili waweze kurithi mali hizo. Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es saalam ametoa kauli hiyo leo Feb 16 mwaka 2026 katika viwanja vya Mnazi mmoja wakati akizindua kamati za kisheria ngazi ya wilaya na mkoa wa Dar es saalam  pamoja na kiliniki ya kisheria iliyoandaliwa na ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali. Kwa sababu mkuu huyo wa mkoa wa Dar es saalam mbali na kuipongeza ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali kwa kutoa huduma  na kusema kuzinduliwa kamati hizo na kiliniki hiyo ya kisheria itapunguza sehemu kubwa ya migogoro katika mkoa wa Dar es saalam. Akizungumza katika hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Kamati hiyo,Mkuu huyo  wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila,ambaye alikuwa mge...