Skip to main content

Posts

Showing posts from September 20, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Majaliwa Kufungua Maonesho Ya Madini Geita

Shoo awataka wadau kujifunza teknolojia mpya za uchimbaji Geita, Septemba 21, 2025 Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini Geita yanatarajiwa kuzinduliwa kesho na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili, Manispaa ya Geita. Akizungumza leo, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, Samwel Shoo, amesema Tume ya Madini inashiriki maonesho hayo kwa mara ya nane mfululizo na imeandaa huduma za elimu kwa wadau wote wa sekta ya madini watakaotembelea mabanda yake. Elimu hiyo itahusu teknolojia za kisasa za utafiti, uchimbaji na uchenjuaji wa madini. “Huu ni msimu muhimu unaowaunganisha wachimbaji, wachenjuaji, wafanyabiashara na wadau wengine wa madini ili kubadilishana ujuzi na kujifunza mbinu mpya. Pia ni nafasi ya kuimarisha uhusiano wa sekta ya madini na sekta nyingine za kijamii na kiuchumi,” amesema Shoo. Ameongeza kuwa ni fursa kwa wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa pamoja na wawekezaji kujifunza teknolojia mbalimbali zinazotumika k...

Makonda ashindwa kujizuia, amwaga machozi madhabahuni

Mgombea Ubunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda ametokwa machozi wakati wa maombi katika Huduma ya Radio Safina lililopo Mbauda jijini Arusha  Makonda alijikuta kwenye hali hiyo I wakati alipopewa nafasi kusalimia kanisani hapo leo Jumamosi 20, 2025 akisema nia yake katika kuwania nafasi hiyo ni kuwatumikia wananchi wa Arusha. Amesema kufanya hivyo ni kutimiza kusudi la Mungu lililopo ndani yake huku akiwaomba waumini kumuombea ashinde awe mbunge katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.  Amesema Taifa linahitaji viongozi ambao watatimiza kusudi la Mungu hapa duniani, wenye maono na wasiotanguliza maslahi binafsi badala yake watekeleza matakwa ya waliowachagua kuwa kwenye mamlaka

Rais Samia anatambua mchango wa madhehebu ya dini katika kuendeleza maarifa - Majaliwa

  *_Asema elimu haiwezi kukamilika kama hakuna maadili._*   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua kwa dhati mchango wa madhehebu ya dini ikiwemo BAKWATA na wadau wote wa elimu katika kuimarisha maadili, kuendeleza maarifa na kuleta mshikamano wa kitaifa kupitia elimu.    Amesema kuwa elimu haiwezi kukamilika kama hakuna maadili kwani ndiyo yanayojenga utu, heshima na mshikamano wa kijamii. "Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha elimu inakuza maarifa na ujuzi, sambamba na malezi yanayoimarisha tabia bora na maadili ya kizalendo kwa vijana wa Kitanzania". Amesema hayo Jumamosi Septemba 20, 2025 alipomwakilisha Rais Dkt. Samia katika hafla ya usiku ya utoaji tuzo za elimu za mufti iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Serena hotel jijini Dar es Salaam. "Rais Dkt. Samia anawapongeza sana BAKWATA kwa juhudi kubwa mnazozifanya katika masuala yote ya maendeleo ya jamii hususan mchango wenu ka...

Mavunde Azisaka Kura za Ccm Jimbo la Mtumba Mtaa Kwa Mtaa

  *KATA YA HOMBOLO MAKULU-JIMBO LA MTUMBA* Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtumba kwa tiketi ya CCM Ndg. Anthony Mavunde ameendelea na awamu ya kwanza ya kampeni yake ya mtaa kwa mtaa kwa kila kata kuzungumza na makundi mbali katika maeneo husika. Ndugu Mavunde ameendelea na ziara yake kata ya HOMBOLO MAKULU na kutembelea na kuzungumza na wananchi wa Mitaa ya ; -𝙈𝙖𝙮𝙚𝙩𝙤 -𝙕𝙚𝙥𝙞𝙨𝙖 𝘼 -𝙕𝙚𝙥𝙞𝙨𝙖 𝘽 -𝙈𝙖𝙨𝙚𝙮𝙖 -𝙆𝙖𝙣𝙜𝙖𝙡𝙞𝙢𝙖 -𝙈𝙨𝙞𝙨𝙞 Ndg. Mavunde pia alitumia fursa hiyo kuwaombea kura Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. Samia S. Hassan na Mgombea Udiwani wa kata ya Hombolo Makulu Ndg. Mokiwa Sahali. 

Ziara ya Mtaa Kwa Mtaa Jimbo la Ubungo Kata ya Makurumla.

Mhe. Prof KITILA MKUMBO ameendelea na Ziara ya kupita mtaa kwa mtaa kwa lengo la kuwaomba KURA Wananchi kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwezi oktoba 29 Mwaka huu.  Vile vile Ziara hiyo hutumika kuwasikiliza Wananchi kero zao na kuwaeleza Yale ambayo yamefanyika na  yanayotarajiwa kufanyika kwa Mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025-2030.  Mhe. Prof Kitila Mkumbo alipokuwa kata ya makurumla aliweza kukutana na makundi mbali mbali yakiwemo Vijiwe vya Boda Boda, Bajaji , viongozi wa Dini, wafanya biashara wa sokoni, wauza vitambaa na washonaji, wauza majeneza pamoja na kufungua Zahanati na Duka la Dawa la Magaye Pharmacy.