Skip to main content

Posts

Showing posts from August 20, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia aongoza Kamati Kuu ya kuteua wagombea ubunge

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,kilichoketi leo Agosti 21,2025 Jijini Dodoma kwa ajili ya kuchukua uteuzi wa Wagombea Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Wabunge wa Viti Maalum,Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Viti Maalum.

Trc Kumwaga Ajira 2,460 Sgr

Shirika la Reli Tanzania linatarajia kuajiri wafanyakazi 2,460 katika mradi wa reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) kwa vipande viwili vya Kutoka Dar es Salaam mpaka Makutopora. Hayo yamebainishwa wakati wa ziara ya siku mbili ya bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC),  Kukagua maendeleo ya ujenzi wa  mradi wa reli ya kiwango cha kimataifa  (SGR ) na MGR, kati ya Kigoma-Tabora  na Tabora  Mwanza iliyoanza Agosti 19, 2025. Ajira hizo ni mbali na zaidi ya ajira 115,000 ambazo tayari zinatokana na mkandarasi katika kipande cha kwanza mpaka cha sita. Katika ajira hizo 2,460 utekekezaji wake ni awamu  ambapo katika mwaka wa fedha 2024/25 zaidi ya watumishi 500 wameshaajiriwa na mwaka huu wa fedha 2025/26 marajio ni kuajiri watumishi 272 na TRC itaendelea kuajiri kufikia watumishi 2,460. Wakati utekekezaji wa utoaji ajira rasmi za Shirika ukiendelea, jumla ya ajira 115,000 kutoka mkandarasi zimeshawanufaisha Watanzania 115,000 zikiwemo za vijana wa ...

Idadi ya Wagombea Urais Uchaguzi Mkuu wa Januari 2026 yafikia zaidi ya 180

Kampala Aliyekuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaabong, Mark Abuku (65), amechukua fomu za uteuzi kutoka Tume ya Uchaguzi jijini Kampala Jumanne, Agosti 19, 2025, akitangaza rasmi nia ya kugombea urais wa Uganda mwaka 2026. Ahadi Zake Kuu Kupunguza gharama za bunge kwa kupendekeza mfumo mpya ambapo kila wilaya itakuwa na mbunge mmoja tu. Kuzindua mpango wa nyumba nafuu kwa wahitimu wapya wa vyuo vikuu. Kupunguza deni la taifa, ambalo limeongezeka kutoka dola za Marekani bilioni 35.1 mwaka 2018/19 hadi dola bilioni 45.8 mwaka 2023/24. Historia Yake Mwaka 2006, Abuku alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kushughulika na fedha bandia, na akashikiliwa gerezani kwa karibu wiki moja. Mchakato wa Uteuzi Mpaka sasa, watu 183 wamechukua fomu za kugombea urais akiwemo Rais Yoweri Kaguta Museveni, Robert Kyagulanyi maarufu Bobby Wine pamoja na Vijana wapatao kumi wa kizazi cha Gen Z.  Fomu zinapatikana kila siku za kazi kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni na zo...

Mwanasheria Mkuu Wa Serikali Ashiriki Utiaji Huu wa Saini....

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari ameshiriki hafla ya utiaji saini Makubaliano ya nyongeza kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya Nyanzaga Mining Company Limited kwa Ajili ya Uchimbaji Mkubwa wa Madini ya Dhahabu. Hafla hiyo imefanyika tarehe 20 Agosti, 2025 katika Kijiji cha Sotta Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza, ambapo Mkataba wa nyongeza kutoka asilimia 16 hadi 20 za umiliki wa hisa za kampuni ya Ubia ya Sotta umesainiwa.  Aidha, mradi huo utagharimu zaidi ya shilingi trilioni 1 na kuufanya kuwa mgodi mkubwa wa Dhahabu kuanzishwa tangu Mwaka 2009.  Kusainiwa kwa mkataba huo ni matunda ya juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuweka mazingira wezeshi ya Uwekezaji.

Kasi Ndogo ya Utekelezaji Mradi Wa Umeme Wa Chalinze - Dodoma Yamkasirisha Dkt. Biteko

📌 Asikitishwa mradi huo aliouzindua Novemba 2024 kuwa nyuma kwa asilimia Saba 📌 Asema Rais Samia alitoa agizo mradi usichezewe kutokana na umuhimu wake katika mikoa mbalimbali ikiwemo ya Magharibi 📌 Asema sababu zilizotolewa na mkandarasi  (TBEA) za kusuasua kwa mradi hazikubaliki 📌 Atoa maagizo kwa Mkandarasi kuwasilisha mpango kazi mpya kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati  ili kufidia muda uliopotezwa 📌 Aagiza TANESCO kutumia mapato ya ndani kulipa fidia wananchi wanaopisha mradi Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze  hadi Zuzu Dodoma na kueleza kutoridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao  ulipaswa kuwa umefikia asilimia 31 lakini kwa sasa  umefikia asilimia 24 tangu kuzinduliwa kwake Novemba mwaka 2024.  Hali ya kusuasua kwa mradi imebainika wakati Dkt. Biteko akikagua mradi huo kat...

Kasi ndogo ya utekelezaji wa mradi wa umeme wa Chalinze - Dodoma wamkasirisha Dkt Biteko

📌 Asikitishwa mradi huo aliouzindua Novemba 2024 kuwa nyuma kwa asilimia Saba 📌 Asema Rais Samia alitoa agizo mradi usichezewe kutokana na umuhimu wake katika mikoa mbalimbali ikiwemo ya Magharibi 📌 Asema sababu zilizotolewa na mkandarasi  (TBEA) za kusuasua kwa mradi hazikubaliki 📌 Atoa maagizo kwa Mkandarasi kuwasilisha mpango kazi mpya kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati  ili kufidia muda uliopotezwa 📌 Aagiza TANESCO kutumia mapato ya ndani kulipa fidia wananchi wanaopisha mradi Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze  hadi Zuzu Dodoma na kueleza kutoridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao  ulipaswa kuwa umefikia asilimia 31 lakini kwa sasa  umefikia asilimia 24 tangu kuzinduliwa kwake Novemba mwaka 2024.  Hali ya kusuasua kwa mradi imebainika wakati Dkt. Biteko akikagua mradi huo kat...

Dk Dotto Biteko kuzindua telnolojia ya kuondoa uvimbe bila upasuaji

  Mwandishi Wetu NAIBU Waziri Mkuu, Dotto Biteko anatarajiwa kuzindua teknolojia mpya ya kuondoa uvimbe mwilini bila upasuaji inayofahamika kama  High-Intensity Focused Ultrasound (HIFU). Uzinduzi wa teknolojia hiyo utafanyika tarehe 26 mwezi huu kwenye hospitali ya Kairuki Mikocheni jijini Dar es Salaam. Hayo yalisemwa jana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kauriki Hospital, Dk Onesmo Kaganda wakati akizungumzia uzinduzi huo. Alisema uzinduzi wa HIFU ni tukio la kihistoria kwakuwa ni mara ya kwanza katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati huduma hii inazinduliwa. Alisema kabla ya kuingia hapa Tanzania, teknolojia hiyo imeanzishwa katika nchi tatu tu za barani Afrika ikiwemo Misri, Nigeria na Afrika Kusini. Alisema HIFU ni Teknolojia ya kisasa inayotumia Mawimbi Sauti (Sound Waves) kutibu aina mbalimbali za uvimbe mwilini bila upasuaji, ikiwemo uvimbe wa saratani na usiokuwa wa saratani katika maeneo kama Matiti, Kongosho, Kizazi kwa Wanawake, na Tezi Dume kwa wanaume. Alit...