Skip to main content

Posts

Showing posts from November 28, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda ashinda kesi ya Kulawiti

  Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza imemuachia huru aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt.Yahaya Nawanda katika Kesi ya kumwingilia kinyume na Maumbile Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine  iliyokuwa ikimkabili. Uamuzi huo wa kesi namba 1883/2024 umetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Erick Marley baada ya kujiridhisha kuwa hakukuwa na ushahidi unaoweza kumtia hatiani Dkt.Nawanda Hakimu Mkazi Mfawidhi Marley amesema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri umeacha shaka katika maeneo mbalimbali ikiwemo Video Mjongeo(CCTV)zilizowasilishwa kutoonyesha sehemu wawili hao walikuwa kwenye gari wakitenda tukio hilo. Jamhuri kutowasilisha vipimo vya vinasaba(DNA)vilivyochukuliwa kwa wawili hao huku katika ushahidi wake Binti aliyedai kulawitiwa na Dkt.Nawanda akidai kufanyiwa ukatili huo kwenye gari nyeupe lakini gari hilo halikuwa nyeupe bali ya Silver. Aidha binti huyo alisema wakati anafanyiwa kitendo hicho,gari lilikuwa na vioo(Tinted)na nje haku...

Waziri Kikwete:Fursa za ajira kwa Vijana nje ya nchi Kipaumbele cha Serikali ya Rais Samia

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kufungua fursa zaidi za ajira kwa watanzania nje ya nchi.  Aidha, Mhe. Ridhiwani amesema serikali inatekeleza mpango wa kuwaandaa vijana kuwa na ujuzi stahiki unao wawezesha kumudu ushindani kwenye soko la ajira la kimataifa sambamba na kufanya kazi zenye tija.  Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo leo Novemba 28, 2024 Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kuwaaga Vijana wa Kitanzania wanaoenda kufanya kazi nchini Saudi Arabia.  Waziri Ridhiwani Kikwete, amebainisha kuwa Serikali imesaini makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya ajira na nchi ya Falme za Kiarabu (UAE), Saudi Arabia, Iran na Qatar kwa lengo la kuongeza fursa zaajira kwa watanzania kwenye nchi hizo. "Serikali imeweka malengo mahususi ya kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania kutoka 556,065 kwa mwaka 2022 hadi 1,00...