Skip to main content

Posts

Showing posts from September 8, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt.Nchimbi Kuwahutubia Wananchi Sumbawanga Mjini

MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi Dkt.Nchimbi Kuwahutubia Wananchi Sumbawanga Mjini kwenye uwanja wa Majengo,Jimbo la Sumbawanga mjini kwa ajili ya kuwahutubia  Wananchi kwenye mkutano wake wa Kampeni leo Septemba 9,2025 mkoani Rukwa.

Mombo Amewagusa Pabaya Walitaka Kuguruga Amani na Utulivu wa Nchi

    Na Mwandishi Wetu;  Dar es Salaam Hivi karibuni kumekuwa na mtiririko wa taarifa mbalimbali za uzushi kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Suleiman Mombo. Taarifa hizo ambazo zinasambazwa kwa nia ovu na genge la watu waliopo nje ya nchi na wengine wa ndani ya nchi, zinafanya upotoshaji mkubwa kuhusu maisha binafsi na kazi ya mkuu huyo wa taasisi hii nyeti. Wapotoshaji hao walianza kwanza kusambaza taarifa za uzushi kuhusu kifo cha mkuu wa usalama wa taifa wa Tanzania. Walivyoona kuwa wameumbuka kuhusu uzushi huo, wakaibua upotoshaji mwingine kuhusu uadilifu wake. Kwa asili ya kazi yake na maadili ya cheo chake, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DGIS) hawezi kuitisha mkutano wa vyombo vya habari kukanusha upotoshaji huo. Mwiko na maadili ya kazi yake yanamtaka akae kimya licha ya shambulio linalofanywa dhidi ya heshima na utu wake. Je, lengo la kampeni hii chafu ya upotoshaji dhidi ya DGIS ni nini ? Jibu la ...

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Yafanya Kikao Cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha imefanya kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa robo ya Aprili hadi Juni mwaka wa fedha 2024/2025, kikao kilicholenga kujadili hali ya lishe mashuleni na utekelezaji wa afua za lishe katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo. Kikao hicho kimefanyika chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, ambaye amewataka watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia ipasavyo utoaji wa chakula chenye lishe bora kwa wanafunzi katika shule zilizopo katika maeneo yao.  Aidha, aliwataka kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa siku za lishe katika mitaa yao ili kuhakikisha jamii inapata elimu sahihi kuhusu umuhimu wa lishe bora. Mhe. Simon amesisitiza kuwa watendaji hawapaswi kubaki ofisini bali wanatakiwa kwenda moja kwa moja mashuleni na kuhamasisha walimu, wazazi na jamii kwa ujumla kushiriki katika juhudi za kuboresha lishe kwa watoto. Akitoa taarifa ya hali ya lishe mashuleni, Afisa Lishe wa Manispaa ya Kibaha Bw. Juma Nzi...

Rais Samia Aimarisha Huduma MOI

Na Mwandishi wetu, Dodoma Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais  wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan  imewezesha Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Famamu Muhimbili (MOI)  kutoa huduma bora za ubingwa bobezi  kwa  ununuzi wa vifaa vya kisasa ikiwemo CT SCAN mbili, MRI, mbili Angio Suite, Ultrasound na X-Ray za kisasa. Hayo yemesemwa leo Septemba 8, 2025 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini MOI Dkt Marina Njelekela wakati akifungua kikao cha pili cha Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi hiyo. "Hili ni jambo la kujivunia na kuishukuru Serikali yetu ya Awamu ya Sita, niwaombe tuendelee kuvitunza na kuvithamini vifaa hivi ili viendelee kuwanufaisha wananchi", alisisitiza Dkt Njelekela Akieleza zaidi Dkt Njelekela amesema  Menejimenti ya Taasisi hiyo iendelee kuwakumbusha watumishi  kufuata misingi ya maadili katika kuhudumia wananchi  kwa kufanya kazi kwa bidii kama wanavyofanya sasa. "Ninafurahi kwamba MOI...

Dk.Nchimbi Awashurukuru Kalambo Kujitokeza Kwa Wingi Mkutano Ccm

Na Mwandishi Wetu MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amewashukuru wananchi wa jimbo la Kalambo kwa kujitokeza kwa wingi katika mkutano wa kuomba kura za mgombea Urais kupitia Chama hicho Rais Dk.Samia Suluhu Hassan. Akitokea jimbo la Kwela,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini,Dkt.Nchimbi  amewashukuru Wananchi wa Jimbo la Kalambo kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano wake wa hadhara wa kampeni.  Pamoja na mambo mengine kwenye mkutano wake wa hadhara,Balozi Dkt.Nchimbi  aliwanadi wagombea Ubunge wa mkoa wa Rukwa akiwemo Mbunge wa jimbo la Kalambo,Edifonsi Joackim  Kanon pamoja na Madiwani. Dk.Nchimbi ameingia Mkoani Rukwa leo kuendelea kusaka kura za kishindo kwa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.

Wananchi wa Kata ya Katerero Waipongeza Serikali Kwa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi

 Na Angela Sebastian;Bukoba Serikali ya hawamu ya sita imewaondolea adha ya kutembea kilometa 15 wanafunzi wa kata ya Katerero iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba kwenda kusoma katika shule ya sekondari ya Bujunangoma iliyopo kata jirani ya Kemondo. Hiyo imetokana na kuwajengea shule ya sekondari inayotoa mafunzo ya amali iliyogharimu shilingi bilioni 584 ambayo imezinduliwa leo na mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa 2025. Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ali Ussi amewataka vijana hususani wanafunzi kuchangamkia fursa hiyo ya Elimu ambayo itawezesha kujiajiri pindi watakapo hitimu masomo yao. Ussi amesema kuwa lengo la Serikali ya hawamu ya sita ni kujenga shule hizo zenye mchepuo wa amali, ni kuwezesha vijana kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira pindi wanapohitimu masomo yao. Aidha emewashauri wananchi wa Halmashauri ya Bukoba kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba 29 mwaka huu ili kuwachagua viongozi watakaowaletea maendeleo ya kweli. Akitoa...