Na. Happiness Sam - Manyara Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) wamepongeza juhudi za Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara katika kuboresha ikolojia ya maeneo yake, hatua iliyochangia ongezeko la wanyama katika Hifadhi hiyo. CPA. Khadija Ramadhani ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi alitoa pongezi hizo leo februari 06, 2025 wakati wa ukaguzi wa maeneo hayo, ukaguzi uliyofanyika ndani ya hifadhi hiyo iliyopo mkoani Manyara. Akiwa katika ziara hiyo CPA. Khadija alisema, “Niwapongeze Menejimenti ya Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara kwa juhudi kubwa za kuboresha mazingira na ikolojia ya maeneo mbalimbali katika Hifadhi hii, hali iliyopelekea ongezeko la wanyama tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali”. Aidha aliongeza, “Leo tumeshuhudia Twiga, Pundamilia, Tembo na Swala wengi, niwapongeze kwa kazi nzuri ya kuendelea kuyalinda maeneo ya Hifadhi zetu na kuboresha maeneo y...
Marato tv - Sauti ya Jamii