Skip to main content

Posts

Showing posts from May 20, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ruvuma Kunufaika Kiuchumi na Makaa ya Mawe

  *Makaa ya Mawe, Vito na Dhahabu kichocheo cha uchumi mkoani Ruvuma* 🔺_Makusanyo maduhuli yafikia asilimia 98 kwa mwaka 2024/2025_ 📍*Ruvuma* MAKUSANYO  ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Ruvuma  yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha  ulioanza Julai 2024/2025 ni Shilingi Bilioni 32.5. Fedha hizo ni makusanyo ya mpaka tarehe 19 Mei, 2025 wakitarajiwa kuvuka lengo la fedha walilopangiwa la Shilingi Bilioni 33.15. Akizungumza na  wanahabari wa Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi amesema, hadi mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu Mkoa huo utakuwa umevuka lengo la zaidi ya  asilimia  100 ya ukusanyaji mapato. Mhandisi Bikulamchi amesema kuwa mafanikio hayo yamepatikana kutokana na kushamiri kwa biashara ya makaa ya mawe ambayo kwa Mkoa wa Ruvuma yamebainika kuwa ni bora zaidi na yamekuwa yakiuzwa nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Bara la Asia na...

Mudavadi atetea Rais Samia kuhusu wanaharakati ‘kuingilia’ masuala ya Tanzania

MKUU wa Mawaziri Nchini Kenya, Musalia Mudavadi ametetea matamshi ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu wanaharakati wa Kenya kuingilia masuala ya utawala nchini mwake. Haya yanajiri huku mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi akiendelea kuzuiliwa Tanzania. Akizungumza Jumanne usiku (Mei 20, 2025) katika Citizen TV, Mudavadi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Kigeni alikiri kwamba maoni ya Rais Suluhu kuhusu wanaharakati “kuingilia” masuala ya Tanzania yanaonyesha ukweli fulani. “Sitapinga hilo kwa sababu nadhani kuna ukweli fulani. Hebu tukabiliane na mambo machache. Kiwango cha adabu, matusi, tunachoona nchini Kenya, ingawa tuna uhuru wa kujieleza, wakati mwingine kinazidi kupita kiasi. Ni ukweli anavyosema kuwa wakati mwingine matamshi yetu huku Kenya hupita kiasi,” alieleza Bw Mudavadi. Aliongeza kuwa Wakenya wakati fulani wanakosa uadilifu katika matamshi yao. “Mimi pia ni Mkenya, na ukweli wa mambo ni kwamba mtazamo wetu na matamshi yetu, kwa sababu tuna uhuru wa kujieleza...

Bwanku Awaongoza Maafisa Takukuru Mkoa Kagera Kufuatilia Eneo La Kijiji Linalodaiwa Kuuzwa Kinyemela

  _Waambatana na Uongozi Serikali ya Kijiji, CCM, Wataalamu wa Kata na Mipango Miji. Waingia poli la kutisha kulipima._  Jana Jumanne Mei 20, 2025 Maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) chini ya Abdallah Kihiyo wakiongozana na Maafisa wa Mipango Miji Mkoa chini ya Adolf Kasa wamefika kwenye Tarafa ya Katerero kufuatilia, kukagua na kupima eneo la kijiji cha Katoju lililopo eneo la Kyanguge, kitongoji cha Mahororo kwenye Kata ya Bujugo linalodaiwa kuuzwa kinyemela na baadhi ya Viongozi wa Kijiji cha Katoju.  Maafisa TAKUKURU na wale wa Mipango Miji waliongozwa na Afisa Tarafa ya Katerero, Bwanku M Bwanku akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Bujugo Twino Felician, Kaimu Mtendaji wa Kata Anthony Babolio, Uongozi wa Serikali ya Kijiji hicho, Viongozi wa Baraza la ardhi na wataalamu wengine ndani ya Kata. Afisa Tarafa Bwanku baada ya kikao kifupi kilichofanyika kwenye Ofisi ya Kijiji, aliwaongoza Maafisa hao wa TAKUKURU na wale wa Mipan...

CBE yapania kukua na kuwa chuo cha kimataifa

Na Mwandishi Wetu CHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kinatarajia kujenga maabara za kisasa zitakazoidhinishwa na mashirika ya kimataifa ya viwango ambazo zitakuwa kitovu cha mafunzo, utafiti, na ushauri wa vipimo katika Afrika Mashariki na Kati. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam  na Mkuu wa chuo hicho, Profesa Edda Lwoga wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya siku ya vipimo duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka. Alisema anaamini kwamba maabara hizo zitachangia maendeleo ya teknolojia na viwanda nchini huku akusema kuwa ndoto ya CBE  ni kuendelea kukua na kuenea zaidi Tanzania na kimataifa. “ Miongoni mwa malengo yetu kwa sasa ni kuanzisha programu mpya za kitaaluma zinazoendana na mahitaji ya sasa kwenye sekta ya vipimo na usanifishaji wa viwango (metrology), ikiwa ni pamoja na kuanzisha shahada  ya Kwanza ya elimu ya Vipimo na Usimamizi wa Ubora (Bachelor in Metrology and Quality Management) ikifundishwa kwa njia ya uanagenzi (apprenticesh...

Waziri Mavunde Aongoza Kikao cha Kimkakati wa Kiuchumi wa Nchi Kupitia Shirika la Madini la Taifa (Stamico)

▪️Lengo ni kuiwezesha Taifa Kushiriki kikamilifu katika uvunaji Rasilimali Madimi kupitia uwekezaji Mkubwa wa STAMICO  ▪️STAMICO kuweka nguvu kubwa katika madini mkakati na adimu ▪️Mapato ya Shirika yatarajiwa kuongezeka kwa asilimia zaidi ya 500 ifikapo mwaka 2029 ▪️Yaja na kauli mbiu mpya ya 𝙈𝘼𝙎𝙏𝘼𝙎𝙃𝘼(𝙈𝙖𝙠𝙚 𝙎𝙏𝘼𝙈𝙄𝘾𝙊 𝙎𝙝𝙞𝙣𝙚 𝘼𝙜𝙖𝙞𝙣) *Dodoma* Shirika  la  Madini la Taifa  (STAMICO) limekaa Mguu Sawa kuhamia kwenye Uwekezaji Mkubwa wa  Madini Muhimu na Madini Mkakati huku tayari likiwa na mafanikio kadhaa ikiwemo kuachana na utegemezi kwa Serikali kwa asilimia 100 na likiwa limekwisha toa gawio kwa Serikali  ya kiasi cha shilingi bilioni 9. Mbali na hayo, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha Shirika hilo linakua kubwa kama ilivyo malengo ya kuanzishwa kwake ya kuwekeza kwa niaba ya Serikali ambapo miongoni mwa majukumu yake ni pamoja na kuwekeza  kwenye miradi ya kimkakati ya utafutaji na uchimbaji madini  ili kuongeza manufaa ...

Rais Samia amesaidia Wachimbaji wadogo wa Madini kupata Leseni

GEITA MJINI: KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Amos Makalla amesema serikali imeazimia kuwainua wachimbaji wadogo wa madini lengo ni kuhakikisha uchumi wa wachimbaji wote unakuwa kwa pamoja. Makalla ameeleza hayo  leo Mei 20 wakati akizungimza na wananchi wa Geita Mjini mkoani Geita, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku saba katika mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Kagera, Geita, Mwanza Simiyu na Shinyanga. Akifafanua hilo Makalla amesema azma ya serikali ikiongozwa na Rais Samia ni kuwajali wachimbaji wadogo wa madini na ndo maana rais wao na wachimbaji wameendekea kumuunga mkono na jitihada zake kwa sababu ameingia kwenye rekodi ya kuwajali wachimbaji wadogo. Ameeleza hilo akisisitiza kuwa wachimbaji wakubwa waliopo alianza kama wachimbaji wadogo, hivyo wachimbaji hao wakipewa fursa wataweza kukua na kuajiri watu na kuongeza mapato na azma ya serikali ya CCM ni kuwajali wachimbaji wote kuhakikisha uchumi una...

Jinsi Serikali ya Kenya inavyowashughulikia Wakosoaji wake

  HATUA ya maafisa wa usalama kuvamia makazi ya Gavana wa Trans Nzoia, wengine kuzingira makazi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na kukamatwa na Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya imeendeleza dhana kuwa serikali imetumia vyombo vya dola kuwaadhibu wapinzani wake. Katika siku za hivi karibuni, viongozi wanaosawiriwa kuwa wakosoaji wa utawala wa Rais William Ruto wamelengwa na asasi za serikali kwa tuhuma za ufisadi na kutoa matamshi ya uchochezi. Hali hii inafanana na enzi za rais mstaafu Uhuru Kenyatta ambapo wakosoaji wa utawala wake na wandani wa Dkt Ruto, aliyekuwa naibu wake, walikamatwa kwa tuhuma za hizo hizo za ufisadi ya uchochezi wa chuki. Kukamatwa kwa wanasiasa hao kulishika kasi zaidi baada ya Bw Kenyatta kutofautiana kisiasa na Dkt Ruto baada ya handisheki yake na kiongozi wa ODM Raila Odinga mnamo Machi 9, 2018. Kando na Bw Gachagua, Bw Natembeya na Bw Salasya, mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi pia anamulikwa na asasi za serikali. Hii ni baada ya kampuni moj...

Rais Samia Amkaribisha Mgeni Wake Rais Namibia Ikulu Dar es Saalam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.

Mkuu wa Majeshi wa Uganda Ampa Tano Rais Samia

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ameonyesha kuunga mkono hatua ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuzuia wanaharakati na mawakili wa Kenya kuingilia masuala ya ndani ya Tanzania.  Muhoozi amemsifu Rais Suluhu kwa kuwa kiongozi mwenye maamuzi thabiti, akisema kuwa anazidi kuwa mmoja wa viongozi anaowapenda barani Afrika.  “Mama Samia Suluhu, rais wa Tanzania, ni miongoni mwa viongozi ninaowaenzi barani afrika. Ni mwenye msimamo dhabiti na hapendi mambo ya kipuuzi. Asante sana Mama”-, alisema katika akaunti yake ya X. Kauli yake inajiri baada ya wanaharakati wa Kenya, akiwemo Martha Karua na Willy Mutunga, kuzuiwa kuingia Tanzania wakitaka kufuatilia kesi ya Tundu Lissu, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uchochezi na uhaini.  Rais Dkt. Samia Suluhu amesisitiza kuwa Tanzania haitaruhusu wageni kuingilia masuala yake ya ndani, akisema kuwa nchi hiyo si “shamba la bibi” ambapo kila mtu anaweza kusema au kufanya anavyotaka bila mipaka...