Skip to main content

Posts

Showing posts from May 17, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miradi ya Maji inaendelea Kujengwa Nchini Kote-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na ujenzi wa miradi ya maji katika maeneo yote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo karibu na makazi yao. Ameyasema hayo leo (Jumapili, Mei 18, 2025) wakati akizungumza na wananchi katika Eneo la Hungumalwa wilayani Kwimba, Mwanza baada ya kuzindua mradi wa maji Hungumalwa akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mwanza. Mradi huo wa maji wa Hungumalwa ulianza kutekelezwa tarehe Machi 08, 2022 na ulikamilika Agosti 15, 2024. Mheshimiwa Majaliwa amewasisitiza wananchi kuendelea kuiamini na kushirikiana na Serikali ambayo imedhamiria kuendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao. Ametaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni pamoja na ya elimu, maji, afya na ujenzi wa barabara. ”Tutaendelea kusimamia maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na tutaendelea kutekeleza ilani kwa vitendo. Kwenye elimu tunaendelea kuk...

Waombaji mikopo ya elimu, tafuteni namba za NIDA mapema

  Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga Ni takwa la kisheria kwa waombaji wa mikopo ya elimu kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwa na namba ya utambulisho (National Identification Number-NIN) au kitambulisho cha uraia kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuweza kuomba mikopo ya elimu. Pamoja na kwamba takwa hilo la kisheria kwa miaka ya nyuma kwa mwombaji ambaye hakuwa na namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia aliweza kuomba na kupata mkopo, lakini kwa mwaka huu wa masomo wa 2025/2026, bila namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia, mwombaji atashindwa kuomba mkopo na hivyo kukosa mkopo. Bodi ya Mikopo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa walifanya mkutano Mei 16, 2025 ambapo mkazo juu ya kila mwombaji  wa mkopo wa elimu kuhakikisha ana namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia uliwekwa bayana mbele ya vyombo vya habari na Watanzania kwa ujumla. Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk. Bill Ki...

Dc Chikoko Aiona Mechi ya Simba na Wananchi Uwanja Wa Mukendo

Na Shomari Binda-Musoma  MKUU wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka usiku wa jana mei 17,2025 ameufatilia mchezo wa timu ya RS Birkane na Simba kwenye uwanja wa shule ya msingi Mukendo Manispaa ya Musoma. Mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa fainali ya kombe la Shirikisho Barani Afrika kati ya timu hizo uliochezwa katika Manispaa ya Birkane nchini Morocco ulishuhudia timu ya Simba ikipoteza kwa kufungwa mabao 2-0. Mkuu huyo wa Wilaya alifunga "projector" ÿa screen kubwa kuwapa fursa wananchi na mashabiki wa soka kufatilia mchezo huo na kupata burudani mbalimbali. Akizungumza kablà ya kuanza kwa mchezo huo mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amesema lengo la kutazama mchezo huo pamoja na kuweka burudani ya muziki ni kuendelea kuufanya mji wa Musoma kuchangamka kwa matukio. Amesema huo ni muendelezo ambao licha ya kuhamasisha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi suala la kula bata na kupata burudani ni sehemu ya maisha kwa wananchi wa Musoma. Mkuu huyo Wilaya ya Musoma amesema kuuch...

Balozi Kombo Awasili Geneva Kuongeza Nguvu ya Kutafuta Kura za Kumchagua Janabi Leo Mei 18

  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amewasili Geneva katika kampeni ya kusaka kura za mgombea wa Tanzania Prof. Mohammed Janabi katika nafasi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO).  Uwepo wake mjini hapo ni ishara na dhamira ya dhati ya kisiasa na mshikamano wa kitaifa, kwani anaungana  na Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jenista Mhagama, na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, kuomba kura kwa  Mawaziri wa Afya kutoka nchi za Afrika. Kwa pamoja, wanatoa wito wa kuunga mkono ombi la Rais Samia Suluhu Hassan la kumchagua kiongozi mwenye maono makubwa aliyejitolea kuboresha na kuimarisha ajenda ya afya barani Afrika.

Makamu wa Rais Amwakilisha Rais Samia Nchini Brazil

Na Ada Ouko, Dodoma. MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Philip Mpango leo mei 17 mwaka 2025 ameondoka nchini kuelekea Nchini Brazil kwa ajili ya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano wa pili unaohusu usalama wa chakula, mapambano dhidi ya njaa na maendeleo vijijini. Mkutano huo wa pili wa Brazil na Afrika unatarajia kufanyika jijini Brasilia kuanzia tarehe 20 hadi tarehe 23 Mei mwaka huu 2025. Aidha mkutano huo utawakutanisha viongozi, wakuu w nchi na serikali, Mawaziri wa kilimo kutoka Afrika, Mashirika ya kimataifa, Benki ya Dunia pamoja na watalaamu mbalimbali. Sambamba na hilo Makamu wa Rais pia anatarajiwa kushiriki katika Mikutano ya Uwili yenye lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania Mashirika na Mataifa yanayoshiriki mkutano huo.

Waziri Mkuu Aridhishwa na Maboresho Yanayoendelea Kwa Mkapa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Mei 17, 2025 amekagua ukarabati wa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kukagua maboresho ya viwanja kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya AFCON na CHAN yanayotarajiwa kufanyika nchini hivi karibuni. Akiwa uwanjani hapo, Mheshimiwa Majaliwa ambaye aliambatana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Gerson Msigwa, amesema ameridhishwa na hatua za ukarabati zinazoendelea kiwanjani hapo.  Waziri Mkuu amesema kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wakandarasi wanaokarabati uwanja huo ni kuwa upo tayari kwa michezo yoyote hata ya kimataifa na kwamba utakamilika kabla ya kuanza kwa mashindano ya CHAN na AFCON. Aprili 7, 2025 Mheshimiwa Majaliwa alikagua ukarabati na ujenzi wa Viwanja vya Amani, Maisara na Mao Zedong Zanzibar, ambapo alisema  Watanzania watapata fursa ya kuendeleza michezo na kuhamasisha wachezaji kufanya mazoezi za...

Kila la Kheri Profesa Janabi Katika Kinyang'anyiro Cha Boss wa Who Ukanda wa Afrika

Uchaguzi wa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unafanyika Mei 18 huko Geneva Uswisi. Mataifa wanachama wanapiga kura katika kikao cha pili maalum cha kamati ya kikanda ya shirika hilo, kumchagua mkurugenzi mpya wa WHO Afrika . Mshindi anakuja kuiziba nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo, Dk. Faustine Ndugulile, waziri wa wa zamani wa afya Tanzania, aliyefariki ghafla Novemba 2024. Janabi ni mmoja wa wataalamu wakubwa wa afya nchini Tanzania, akiwa pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof Janabi ni mgombea pekee kutoka nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, huku wagombea wenzake wakitokea nchi za Afrika Magharibi. Mkurugenzi wa Kanda anachaguliwa kwa kura ya siri katika kikao cha ndani cha Kamati ya Kanda ya WHO kwa Afrika, ambayo ilikutana Januari 14, 2025, na kuamua kutumia utaratibu wa haraka, kumpata Mkurugenzi wa Kanda badala ya mchakato wa kawaida ambayo huchukua muda mrefu. Mkurugenzi huyo anatarajiwa kuhudumu ...

Rasmi Sasa Rais Samia ni Mpiga Kura Wewe Je?

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonyesha kadi yake ya mpiga kura mara baada ya kushiriki zoezi la uboreshaji wa taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo tarehe 17 Mei, 2025 katika Ofisi ya Serikali ya Kijiji, Chamwino mkoani Dodoma.  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki zoezi la uboreshaji wa taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo tarehe 17 Mei, 2025 katika Ofisi ya Serikali ya Kijiji, Chamwino mkoani Dodoma ambapo pia aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari hilo. Mapema Rais Samia alitumia usafiri wa Treni ya SGR kutoka Dar es saalam hadi Dodoma kuja kushiriki katika zoezi hilo ili aweze kupata haki yake ya msingi ya kupiga Kura katika uchaguzi unatarajiwa kufanyika badae mwaka huu wa Madiwani,Wabunge na Rais

Msajili wa Vyama Vya Siasa Ana Mamlaka ya Kutengua Uteuzi wa Chama Chochote Cha Siasa Kwa Mujibu wa Katiba, Sheria na Kanuni

Na David Maphone. Nimemsikiliza vizuri Makamu Mwenyekiti Mhe, John Heche, Katibu Mkuu John Mnyika pamoja na Mjumbe wa Baraza kuu la Chadema Godbless Lema kwa nyakati tofauti wakipinga maamuzi ya Msajili wa vyama vya siasa. KUTENGUA Uteuzi uliofanywa KIMAKOSA na Baraza kuu la Chadema 2025 Mlimani city D'Salaam. Lakini pia nimewasikiliza baadhi ya wanasheria wao wakidai Kwamba Msajili wa vyama hana mamlaka ya Kisheria KUTENGUA UTEUZI wa Chama Cha siasa . Kwa kuwa suala hili limetolewa Kauli pia na   wanasheria wa Chadema na Mwanasheria William Maduhu wa LHRC kwa UPOTOSHAJI huu nimeona muhimu Watanzania wafahamu ukweli wa uongo huu. Kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya siasa Sura Namba 258 Ibara 22 (1)"The Minister may make regulations for the purpose of carrying out OR giving effect to any PROVISION of this Act." Kwa kuwa Ofisi ya Msajili wa vyama ipo kwa mujibu wa Katiba, Sheria na KANUNI na tumeona hapo juu. Kanuni zipo kwa mujibu wa Sheria. Ibara 22 (1) hivyo basi, Mamlaka ...