Skip to main content

Posts

Showing posts from March 26, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Nilijiapiza kujenga shule ya Msingi Misufini bila fedha ya serikali

📍 Asema nadhiri aliyoweka ilitokana na watoto kusoma umbali mrefu 📍 Asema alipokosa fedha serikali alianzisha msalagambo kusaka marafiki zake kutimiza nadhiri yake 📍 Awashukuru CRDB Benki, Karimjee Foundation kumsaidia kujenga madarasa mawili na vyoo 📍 CRBD yaungana na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumpongeza MwanaFA kwa kazi nzuri anayofanya Muheza  📍 Mtendaji wa Kijiji Ataka umbali waliokuwa wakisoma watoto wa Kijiji cha Misufini  📍 Wazazi Misufini Wasema hawakukosea kumchagua MwanaFA kuwa mbunge, wamtaja pia Rais  Na Mwandishi Wetu, Magoroto  NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA, alisema alijiapiza na kuweka nadhiri ya kujenga shule ya msingi katika Kijiji cha Misufini kilichopo kata ya Magoroto kilichokuwa kikikabiliwa na changamoto lukuki. Sambamba na nadhiri hiyo, MwanaFA hakutegemea kama wananchi wa Kijiji hicho wangekichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwakuwa walikabiliwa na changamoto nyingi. Alisema Kijiji ...

Ni "Upuuzi" Kumdai Mh Waziri Mkuu Majaliwa Maendeleo ya Wana-kusini Pekee!

Nimesoma andiko moja kwenye mtandao wa Jamii Forum ambalo naweza kuliita andiko la "kipuuzi" sana ambalo linapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani linajenga picha kuwa Viongozi wetu wa ngazi za kitaifa wanawajibika kupendelea maeneo yao(kwao)kwanza kabla ya maeneo mengine ya Nchi! "Waziri Mkuu Ana "Legacy " Gani ya Kujivunia Kwa Watu wa Kusini?" Kwa kumbukumbu zangu,karibia mwezi wote March,2025,Mh Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekuwa katika ziara za mikoani katika kuwahudumia Watanzania wote kwa Ujumla wao!Sijui ni lini Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa amefanya ziara ya Kiserikali/Kikazi Mkoani Lindi au Mtwara! Ndani ya wiki moja hii Waziri Mkuu Majaliwa nimemuona kupitia TV katika Mikoa ya Tabora badae Mkoani Njombe na leo alikuwa Mkoani Kilimanjaro!Sitoshangaa kesho nikisikia yupo Dodoma au Mkoani Katavi au Kigoma! Nini NATAKA KUSEMA? Mh.Waziri Mkuu ni moja wa viongozi wanne wa juu kabisa kwenye ngazi ya Kitaifa!Mh Waziri Mkuu kabla ya yote kwanza anawajibik...

No Reforms No Election Mara, Ujumbe Wafika Kwa Baba Wa Taifa

Na Shomari Binda-Butiama MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa mara Mwalimu Chacha Heche amefika kwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa na ujumbe wa viongozi wa mkoa na wilaya ya Butiama. Kiongozi huyo amefanya mazungumzo na familia ya Baba wa Taifa ikiwa ni pamoja na kutambulisha uongozi mpya wa Chadema mkoa wa Mara kwa familia hiyo. Licha ya kutambulisha uongozi amewasilisha vielelezo vya matukio yaliyojitokeza katika chaguzi za Tanzania 2019-2024 mkoa wa Mara  Katika taarifa aliyowasilisha Mwenyekiti huyo imesheheni vielelezo vya mauaji kwenye chaguzi,utekaji kwenye chaguzi,majeruhi,kura fake,ubambikaji kesi nyakati za uchaguzi ,ukiukwaji was sheria nyakati za uchaguzi na uenguaji hovyo wa wagombea. " Tunashukuru kwa mapokezi ambayo tumeyapata hapa nyumbani maana hii ni familia yenye heshima kwenye taifa letu. " Tumekuja kutambulisha uongozi wa mkoa wa chama pamoja na Wilaya ya Butiama pamoja na kuzungumzia masuala ya ki...

Sagini Ataka Maafisa Biashara Kuhamasisha Watu Kufungua Biashara na Sio Kufungia Biashara

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amewataka Maafisa biashara kuhamasisha wananchi kuanzisha biashara na sio kufungia biashara kama wanavyolalamikiwa. Akizungumza Katika ziara yake ya Usomaji Utekelezaji wa Ilani kipindi cha miaka minne kwa viongozi wa Matawi ya Mwanzaburiga, Singu, Nyamisisi na Kiabakari katika Kata ya Kukirango, Wilaya ya Butiama amesema kuwa malalamiko mengi kutoka kwa wananchi ni kuhusu maafisa biashara kutoka halmashauri kutuhumiwa kukwamisha biashara. "Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  imekuwa ikijitahidi kuwaandalia mazingira mazuri wafanyabiashara pamoja na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa ulipaji kodi hivyo sioni umuhimu wa kuwadidimiza na tabia hii isipokemewa mapema itafikia kipindi watakata tamaa ukifikiria wengine ndio wanajitafuta," amesema Sagini. Pia Diwani wa Kata ya Kukirango Mhe. Rajab Mjengwa kwa niaba ya wananchi alimpongeza Mbunge Sagini kwa mwendele...

Wauguzi imarisheni Usimamizi wa Utoaji wa Huduma Bora za Afya Nchini - Dkt Dugange

OR-TAMISEMI   Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Dkt. Festo Dugange amewaelekeza Wauguzi Viongozi wa ngazi zote za afya nchini  kuhakikisha wanaimarisha usimamizi wa utoaji wa huduma bora ili wananchi wote wapate huduma bora na kwa usawa.  Dkt. Dugange ameyasema hayo leo Machi 27, 2025 wakati akifungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa wauguzi viongozi uliofanyika katika ukumbi wa  Mikutano wa PSSSF  Jijini Dodoma wenye kauli mbiu ya inayosema HUDUMA BORA WAJIBU WANGU. Amefafanua kuwa Serikali ya Awamu ya sita imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hivyo  bila ya kuwepo kwa  huduma nzuri na bora kutoka kwa watoa huduma za afya, na hasa Wauguzi, uwekezaji huu hautakua na manufaa. “Serikali imefanya uwekezaji mkubwa  kwenye sekta ya afya ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya afya, ununuzi wa vifaa na vifaa tiba, uboreshaji wa mazingira ya kazi, hivyo mapaswa kuwasimamia waliopo chini yenu ili wafanye kazi ...

Kambarage Wasira Aichangua Halmashauri ya Mji wa Bunda

Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Uchumi,fedha na Mipango CCM wilaya ya Bunda Ndg.KAMBARAGE MASATO WASIRA Amekabidhi Truck suit 140  Kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mji wa Bunda Kwa ajili ya Maandalizi ya Mashindano Umitashumita.   vifaa hivyo vyenye Thamani ya Shilingi  Zenye Tathamani ya Milioni Tatu Laki Sita (3,600,000/=) Kwa niaba yake na Ndg MASATU BURE SALUM. 

Rais Samia Atoa Mkononl Wa Pole Milioni Mia Kwa Wananchi Walioathiriwa na Mvua Mjini Musoma

RAIS  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt Samia Suluhu Hassan atoa kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya wananchi waliothiriwa na mvua ilionyesha juzi usiku na kusababisha maafa makubwa katika baadhi ya maeneo ya mji wa Musoma. Mkuu wa mkoa wa Mara kanali Evans Mtambi amepokea kiasi cha fedha ili kiweze kuwasaidia wananchi ambao wamekumbwa na janga hilo. Katika tukio hilo zaidi ya kaya mia tatu zilikosa makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na nyingine kubomolewa,huku majengo ya taasisi kama shule na miundombinu ya umeme na simu vikiathiriwa na mvua hiyo iliyoambata na na upepo mkali usiku wa kuamkia machi 23 mwaka huu.

Rais Ruto Amfuta Kazi Waziri wa Utumishi wa Umma Justine Muturi

 Rais wa Kenya William Ruto amemteua Mbunge wa Mbeere Geoffrey Kiringa Ruku kuwa Waziri wa Utumishi wa Umma kuchukua nafasi ya Justine Muturi. Kwa miezi kadhaa sasa, Muturi ameibuka kuwa mwiba kwa Rais Ruto kutokana na mzozo wake na bosi wake ukihusisha matamshi makali aliyotoa dhidi ya Serikali kuhusu utekaji nyara na mauaji ya waandamanaji wa Gen Z mnamo Juni na Desemba 2024, ambapo mwanawe pia alikuwa mwathiriwa. Muturi Hata alikuwa ameomba kutoshiriki vikao vya Baraza la Mawaziri hadi masuala ya utekaji nyara wa polisi na mauaji ya kiholela yawepo kwenye ajenda. Hivi majuzi, Muturi alisema kwa ujasiri kwamba hatua ya kumwita Ruto bosi wake iko chini ya mamlaka aliyoapishwa kama mtumishi wa umma, na badala yake anafaa kupongezwa kwa hilo. Ruto, ambaye alikuwa amekaa kimya kuhusu suala hilo kwa wiki kadhaa, alivunja ukimya wake Jana Jumanne na kumtaja Waziri wake wa Utumishi wa Umma kuwa "hafai". Akiongea wakati wa hafla ya chakula cha jioni katika Ikulu ya Nairobi, Ruto al...

Rais Samia Apokea Ujumbe wa Rais Wa Drc Ikulu Dar es Salaam

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Félix Antoine Tshisekedi ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi hiyo Mhe. Thérèse Kayikwamba Wagner, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Machi, 2025.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini Awavisha Nishani Kanda ya Mbeya

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan amewavisha nishani mbalimbali Maafisa na Askari wa JWTZ jijini Mbeya leo tarehe 26 Machi 2025. Akizungumza baada ya kuvisha nishani hizo, Jenerali Mkunda amewapongeza Maafisa na Askari waliotunukiwa nishani hizo kwa namna Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyotambua mchango wao katika kulitumikia taifa kwenye nyanja ya Ulinzi. Aidha,amewataka Maafisa na Askari kuendelea kuviishi viapo vyao na kuhakikisha mipaka yote ya nchi yetu inakuwa salama wakati wote. Nishani hizo ni Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Nne,Nishani ya Utumishi Uliotukuka,Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema,Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ na Nishani ya Jumuiya ya SADC.