Anaandika Godbless Lema kwenda kwa Mbowe. Kwako Mh Freeman Mbowe. Kwa heshima, huzuni na uzito wa dhamira, nakuandikia barua hii si kwa hasira, bali kwa mwangwi wa historia inayolilia uaminifu. Tulisimama nyuma yako kwa gharama kubwa kipindi chote ambacho tulikuamini kuwa kiongozi wa matumaini ya kizazi kilichojitoa kwa ajili ya Tanzania mpya ulipokuwa Mkti wetu. Leo hii umetazamwa ukihudhuria mkutano wa Serikali kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa, huku mwenyekiti wetu, Tundu Lissu, akiwa gerezani akikabiliwa na mashtaka ya uhaini na Chama chetu hakiruhusiwi kufanya siasa na wanachama wetu wanapotea, wanateswa, wengine wameuawa na bado hujatokea hata mara moja mahakamani, wala kutoa neno la kukemea udhalimu huu unaoendelea mbele ya macho ya Watanzania. Tulikuwa pamoja nawe wakati ulipokamatwa na kushtakiwa kwa ugaidi na changamoto mbali mbali nyingi katika uongozi wako. Tulilia. Tulipiga kelele. Tulivunjwa. Tukateswa. Lakini tuliendelea kusimama kwa ajili yako kwa sababu tuliamini ...
Marato tv - Sauti ya Jamii