Watu wanne wamekamatwa na madini ya vito katika mtaa wa Togo, Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, kufuatia operesheni maalum iliyofanywa na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mahenge kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Ulanga na uongozi wa Wilaya. Akizungumza na waandishi wa habari mapema jana kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi – Mahenge, Jonas Mwano, alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya taarifa za intelijensia kuonyesha uwepo wa biashara ya madini inayofanyika kinyume cha sheria katika makazi ya watu. Alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha rasilimali za madini zinalindwa na kunufaisha taifa kupitia mfumo rasmi wa masoko. Watuhumiwa hao walikamatwa na madini mbalimbali yakiwemo Spinel, Rhodolite, Tourmaline na Volcanic Glass. Madini hayo yalipatikana nyumbani kwa mmoja wao ambaye pia alikutwa akifanya usanifu wa madini bila kuwa na Leseni ya Usanifu wa Madini kinyume cha Sheria ya Madini Sura 123. Alisema baad...
Marato tv - Sauti ya Jamii