Skip to main content

Posts

Showing posts from December 6, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Watuhumiwa Wanne Wakamatwa na Madini ya Vito Mahenge

Watu wanne wamekamatwa na madini ya vito katika mtaa wa Togo, Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, kufuatia operesheni maalum iliyofanywa na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mahenge kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Ulanga na uongozi wa Wilaya. Akizungumza na waandishi wa habari mapema jana kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi – Mahenge, Jonas Mwano, alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya taarifa za intelijensia kuonyesha uwepo wa biashara ya madini inayofanyika kinyume cha sheria katika makazi ya watu.  Alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha rasilimali za madini zinalindwa na kunufaisha taifa kupitia mfumo rasmi wa masoko. Watuhumiwa hao walikamatwa na madini mbalimbali yakiwemo Spinel, Rhodolite, Tourmaline na Volcanic Glass.  Madini hayo yalipatikana nyumbani kwa mmoja wao ambaye pia alikutwa akifanya usanifu wa madini bila kuwa na Leseni ya Usanifu wa Madini kinyume cha Sheria ya Madini Sura 123. Alisema baad...

Mbunge wa Bukoba Mjini Awapa Kibarua Wanahabari

  Na Angela Sebastian ;Bukoba MBUNGE wa Jimbo la Bukoba Mjini mkoani Kagera Mhandisi Johnston Mutasingwa,amewashauri waandishi wa habari wa Manispaa ya Bukoba kuibua habari za uchambuzi juu ya changamoto zinazowakabili wananchi ili zijulikane na kutafutiwa ufumbuzi wa kina. Pia amewaomba watoe ushirikiano kwa viongozi walioko madarakani kisha kuitangaza miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kwa kuandika habari za mwendelezo ili jamii itambue miradi hiyo imefikia hatua gani na faida zake ni zipi kwasababu, inatekelezwa kutokana na kodi za wananchi. Mutasingwa amesema hayo leo wakati akizungumza waandishi habari mjini Bukoba na kusema kwamba, umuhimu wa ushirikiano huo ni kuhakikisha kuwa habari zinazotolewa zinasaidia jamii kupata taarifa sahihi na za kina kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo. "Nyie ni wanataaluma ya habari tutumie kalamu zetu kuibua habari zenye kuvutia wasomaji na watazamaji,tuwe na mwendelezo mfano, umeandika habari inayohusu ujenzi ...