Rais mteule Donald Trump amemteua mwenyekiti-mwenza wa timu yake ya kampeni, Susie Wiles, kuwa White House Chief of Staff wa Marekani
Rais mteule Donald Trump amemteua mwenyekiti-mwenza wa timu yake ya kampeni, Susie Wiles, kuwa White House Chief of Staff wa Marekani. Anakua mwanamke wa kwanza kuhudumu katika nafasi hiyo. Nafasi ya WH Chief of Staff ni moja ya nafasi zenye ushawishi mkubwa katika utawala wa Marekani, ambapo mhusika huyu hutumika kama mshauri mkuu wa rais na kuhakikisha utendaji wa Ikulu unafanyika kwa ufanisi. Haya ni baadhi ya majukumu ya nafasi hii: 1. Ratiba na Mipangilio: Anasimamia ratiba ya kila siku ya rais, akihakikisha kuwa mikutano na majukumu yote yanazingatia malengo ya utawala. 2. Mshauri na Mlinda Mlango: Akiwa mshauri wa karibu zaidi wa rais, anahusika na kuchuja taarifa na watu wanaofika kwa rais ili kuhakikisha muda na nishati ya rais vinatumika vyema. 3. Mkurugenzi ya Sera na Watumishi: Anasimamia washauri wakuu na watumishi wa Ikulu, akihakikisha kuwa wote wanashirikiana katika kufanikisha ajenda na sera za rais. 4. Kujenga Mahusiano Muhimu: Akitumika kama kiunganishi kati ya ...