Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Ziwa, kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, hii leo imeendesha mafunzo maalumu kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii pamoja na makundi maalumu kuhusu namna ya kujiunga na Mfumo wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya Kielektroniki (NeST) na fursa zinazopatikana kupitia mfumo huo katika ununuzi wa umma. Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wanawake, vijana, wazee na watu wenye ulemavu ambao ni raia wa Tanzania ili waweze kushiriki kikamilifu katika zabuni za Serikali kupitia mfumo wa NeST, sambamba na utekelezaji wa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 na Kanuni zake za mwaka 2024 zinazozitaka taasisi nunuzi kutenga asilimia 30 ya thamani ya ununuzi wao wa mwaka kwa makundi maalumu. Kupitia mfumo wa NeST, makundi maalumu yatapata fursa ya kushiriki katika zabuni mbalimbali za Serikali ikiwemo huduma za ujenzi, usafi wa mazingira, ulinzi na usalama kazini pamoja na huduma zinazohitaji ujuzi, teknolojia na uzoefu, fursa hizi zina...
Marato tv - Sauti ya Jamii