Skip to main content

Posts

Showing posts from September 15, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DKT. KIRUSWA ATATUA MGOGORO WA WACHIMBAJI WADOGO MWANZA

 *Ukosefu wa mawasiliano chanzo cha mgogoro wa wabia katika leseni 33* *Wachimbaji watakiwa kuweka mifumo ya wazi ya ushirikiano na mawasiliano* *Serikali yaonya leseni zisizoendelezwa kufutwa* 📍*Mwanza* Ukosefu wa Mawasiliano na taarifa sahihi miongoni mwa wamiliki wa leseni za uchimbaji madini unaweza kuchochea migogoro isiyo ya lazima na kudhoofisha shughuli za uchimbaji, hasa kwa wachimbaji wadogo. Hayo yamebainishwa leo Septemba 15, 2026 jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akiongoza kikao cha kutatua mgogoro uliowahusisha wachimbaji wadogo jijini humo. Dkt. Kiruswa amesema mgogoro huo umetokana kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa taarifa sahihi na mawasiliano baina ya wabia wanaomiliki kwa pamoja leseni 33, ambapo upande mmoja uliamini kuwa baadhi ya wabia wanafanya uzalishaji bila kumshirikisha na bila kumpatia stahiki zake, huku upande mwingine ukieleza kuwa katika leseni hizo bado haujaanza uzalishaji. Baada ya kusikiliza pande zote, Dkt. Kirus...

RC SAGINI AKUTANA NA MAJESHI YA TANZANIA NA MALAWI KUJADILI HALI YA USALAMA/ ASISITIZA ULIPAJI KODI

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Jumanne Abdallah Sagini amewataka Wananchi wa Mkoa wa Mbeya hasa Wafanyabiashara kuendelea kulipa kodi stahiki kwa mjibu wa Sheria ikiwemo kutoa risiti na unapotoa huduma na kudai risiti baada ya kununua ili kuendelea kuchochea uchumi utakaosaidia kujenga na kuboresha miradi ya Maendeleo ndani ya Mkoa wa Mbeya. Mhe. Sagini amesema Miradi mbalimbali inayotekelezwa mkoani Mbeya inategemea Uwepo wa Uchumi na ni Makusudio mema ya Serikali kuhakikisha uchumi unaimarika katika viwango vya Nchi na hata Uchumi wa Mtu mmoja mmoja na viwango vyote vinategemea ukusanyaji Mapato. Ameyasema hayo leo wakati wa hotuba yake ya Ufunguzi katika kikao cha Ujirani mwema kati ya Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania na Malawi yaliyoketi kwa lengo ya kujadili hali ya Usalama na uimarishwaji wa Amani kati ya Nchi hizi hususani kwa mikoa ya Nyanda za juu kusini inayopakana na Nchi ya Malawi. Aidha Mhe. Sagini amewaomba wananchi Kuchukua tahadhari dhidi ya Mvua za El- nino zi...

PANGANI NA NEEMA YA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA KUCHAKATA MADINI YA MCHANGA WA BAHARINI

 NA: DK. REUBENI LUMBAGALA  Sekta vya viwanda ni injini ya maendeleo ya uchumi kutokana na kufungamanishwa kwake na fursa mbalimbali za maendeleo. Katika jitihada za kuinua maendeleo ya watu na ya uchumi, viwanda havipaswi kuachwa nyuma kwani vina mchango mkubwa katika kufanikisha azma hiyo. Nchi nyingi zilizoendelea zilifanikiwa katika mipango ya maendeleo kutokana na kuipa msukumo mkubwa sekta ya viwanda. Katika mikakati ya kujenga na kuinua uchumi wa Tanzania, serikali imeweka mazingira bora na wezeshi kwa ajili ya uwekezaji za viwanda huku seta binafsi ikipewa nafasi kubwa ya kuwekeza katika viwanda. Mkoa wa Tanga umekuwa na historia kubwa nchini kwa kuwa na maendeleo makubwa ya viwanda, lakini katika miaka ya nyuma viwanda vingi vilikufa. Juhudi za makusudi zimekuwa zikifanywa na serikali kwa kuhakikisha viwanda vilivyokufa vinafufuliwa huku ujenzi wa viwanda vipya ukifanyika kwa kuishirikisha kikamilifu sekta binafsi. Sasa ni dhahiri maamuzi ya kuurejesha mkoa wa Tanga k...

UDOM YAKABIDHI AI ULTRASOUND KWA VITUO 32 DODOMA

Na Mwandishi Wetu - Dodoma Tanzania imeendelea kupiga hatua katika matumizi ya Akili Unde ambapo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimekabidhi vifaa vya kisasa vya upimaji wa mama wajawazito, vinavyotumia teknolojia ya AI Ultrasound kwa vituo 32 vya kutolea huduma za afya katika mkoa wa Dodoma vyenye thamani ya shilingi milioni 352. Hatua hiyo imefanyika leo Spetemba 15,2026 katika kituo cha afya Mkonze Jijini Dodoma, kupitia Mradi wa SAFARI, unaolenga kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto kwa kutumia teknolojia na kuongeza uwezo wa wahudumu wa afya katika kufanya uchunguzi wa wajawazito. Akizungumzia hatua hiyo Mkuu wa mkoa huo Rosemary Senyamule amesema hatua hiyo itaongeza uwezo wa vituo hivyo vya afya kutoa huduma bora za uchunguzi bila mgonjwa kusafiri umbali mrefu kwaajili ya uchunguzi wa afya ya mama na mtoto. "Vifaa hivi vitatumika kama chombo cha awali katika vituo vyetu vya afya, mama mjamzito atakayegundulika kuwa na viashiria vya changamoto au matatizo yoyote wakati wa...

TAASISI YA OMDTZ YAWEZESHA KATA TANO KUWA NA MIPANGO YA KUKABILI MAFURIKO DAR ES SALAAM

 Na Mwandishi wetu – Dar es Salaam Taasisi ya OpenMap Development Tanzania (OMDTZ) kwa kushirikiana na Serikali imeanza zoezi la kukabidhi Mipango ya Kata ya Kujiandaa na Kukabiliana na Mafuriko kwa jamii katika kata tano za Jiji la Dar es Salaam.  Zoezi hilo la siku tano kuanzia tarehe 14 hadi 18 Septemba 2026 ambalo litaziwezesha Kata kupokea mpango na elimu kwa lengo la kuzijea uwezo wa kukabiliana na mafuriko endapo yatatokea katika maeneo yao. Zoezi hilo linalotekelezwa kupitia Mradi wa “Ramani Zetu, Sauti Zetu”, unaofadhiliwa na Zayed Sustainability Prize, linahusisha Kata za Keko, Makurumila, Mabibo, Ubungo na Tabata, na linalenga kuwezesha jamii na viongozi kuwa na mipango na taarifa sahihi za maeneo yao kwa ajili ya maandalizi na mwitikio wa mafuriko. Akifungua rasmi zoezi hilo katika Kata ya Keko, Diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Ismail Amanzi alieleza umuhimu wa mipango hiyo kutumika kama nyenzo ya vitendo katika kuimarisha maandalizi ya jamii na kupunguza athari za m...