Kenya imethibitisha jumla ya visa 314 vya ugonjwa wa Mpox kufikia Julai 31, 2025, ikiwa ni ongezeko kubwa la maambukizi mwaka mmoja tangu kisa cha kwanza kugunduliwa katika mpaka wa Taita-Taveta, Waziri wa Afya Aden Duale ametangaza. Mlipuko huo ulianza Julai 31, 2024, pale mtu aliyekuwa akisafiri kutoka Uganda kuelekea Rwanda kupitia Kenya alipogunduliwa kuwa na Mpox katika kituo cha mpaka cha Taita-Taveta. Tangu hapo, ugonjwa huo umesambaa hadi kaunti 22 licha ya juhudi kabambe za kudhibiti maambukizi zinazoendeshwa na Wizara ya Afya. Kaunti ya Mombasa inaongoza kwa kuwa na visa vingi zaidi vya Mpox, ikirekodi visa 146, ikifuatiwa na Busia (63), Nakuru (21), Kilifi (19), Nairobi (17), na Makueni (13). Taita-Taveta na Uasin Gishu zimeripoti visa vitano kila moja, huku Bungoma ikiwa na visa vinne. Kaunti za Kajiado, Kakamega na Kiambu kila moja imerekodi visa vitatu. Kaunti za Kericho na Machakos zimeripoti visa viwili kila moja, ilhali Migori, Kisii, Kirinyaga, Isiolo, Kitui, Na...
Marato tv - Sauti ya Jamii