Na Mwandishi Wetu, Arusha Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) chini ya menejimenti ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, yakihusisha shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na utoaji wa huduma za matibabu bure kwa wananchi. Maadhimisho hayo, ambayo hufanyika kila tarehe 15 Mei kila mwaka ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa huduma za uuguzi duniani Florence Nightingale, yaliwakutanisha wauguzi kutoka maeneo mbalimbali nchini katika viunga vya Hospitali ya ALMC. Kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo, wauguzi pamoja na madaktari bingwa walitoa huduma za matibabu bure kwa wakazi wa jiji la Arusha kupitia vituo maalum vilivyowekwa katika Hospitali ya ALMC na Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC). Zaidi ya wananchi 1,400 walipata huduma mbalimbali za uchunguzi wa afya hususan magonjwa yasiyoambukiza, huku wauguzi 600 nao wakinufaika na huduma hizo, na ku...
Marato tv - Sauti ya Jamii