Skip to main content

Posts

Showing posts from July 1, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SERIKALI YATENGA BILIONI 38 KUPIMA VIJIJI VYOTE TANZANIA, YAAGIZA KLINIKI ZA ARDHI KILA KATA

  Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, ametangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia utoaji wa kiasi cha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kupima vijiji vyote nchini ili kumaliza migogoro ya ardhi. Mhe. Mmuya amebainisha hayo leo, Julai 1, 2026, katika viwanja vya Sokoni Mugumu wilaya ya Serengeti mkoani Mara, alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi, zikiwemo zile za sekta ya ardhi. Katika hatua ya haraka ya kusogeza huduma kwa wananchi, Mhe. Mmuya amemuagiza Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Mkoa wa Mara pamoja na timu yake, kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha kliniki za ardhi katika kila kata na kila wilaya ya mkoa huo. "Hakikisheni mnaratibu uwepo wa kliniki za ardhi katika kila kata, kila wilaya ili muwasikilize wananchi hawa n...

MLIPUKO WA BARUTI WAUA MMOJA,WAJERUHI SABA NYAMAGANA

Na Dawati la Habari Polisi; Mwanza. Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine saba wakijeruhiwa kufuatia mlipuko wa baruti uliotokea leo Julai 1, 2026, majira ya saa 12:46 asubuhi katika kibanda cha kahawa kilichopo Mtaa wa Sahwa ya Juu, Kata ya Lwanhima, Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa, amesema aliyefariki ni Marco Msenyere (52), mpasua mawe na mkazi wa Semba-Lwanhima. Amesema marehemu alikuwa amefika katika kibanda hicho kunywa kahawa akiwa na begi dogo lililokuwa na baruti. Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mlipuko huo ulisababishwa na uzembe wa utunzaji wa baruti, baada ya marehemu kuweka begi lenye baruti karibu na jiko la mkaa lililokuwa linawaka. Joto kutoka kwenye jiko hilo lilisababisha baruti kulipuka. Majeruhi wa tukio hilo ni Daudi Joseph Baraka (54), Emmanuel Luhangwa Joseph (40), Yusufu Rajabu Nasoro (20), Zawadi Saimon Ndukeji (27), James Husse...

WAZIRI MKUU: SERIKALI KUHARAKISHA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imeweka mkakati wa kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na miradi inakamilika kwa wakati. Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Sokoine, wilayani Serengeti, mkoani Mara, leo Jumatano (Julai 1, 2026), Waziri Mkuu alisema Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/2027 pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.  "Tunaanza utekelezaji wa Ilani leo, Ilani ya 2025–2030. Tunaanza utekelezaji wa Bajeti leo ya mwaka 2026/2027, na tunaanza utekelezaji wa Dira mpya ya 2050 leo. Waziri Mkuu alisema baadhi ya miradi ya maendeleo ilichelewa kuanza au kupungua kasi ya utekelezaji kutokana na uamuzi wa kimkakati wa Serikali wa kuelekeza rasilimali katika kukamilisha miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere, Daraja la JPM na...