Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, ametangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia utoaji wa kiasi cha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kupima vijiji vyote nchini ili kumaliza migogoro ya ardhi. Mhe. Mmuya amebainisha hayo leo, Julai 1, 2026, katika viwanja vya Sokoni Mugumu wilaya ya Serengeti mkoani Mara, alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi, zikiwemo zile za sekta ya ardhi. Katika hatua ya haraka ya kusogeza huduma kwa wananchi, Mhe. Mmuya amemuagiza Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Mkoa wa Mara pamoja na timu yake, kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha kliniki za ardhi katika kila kata na kila wilaya ya mkoa huo. "Hakikisheni mnaratibu uwepo wa kliniki za ardhi katika kila kata, kila wilaya ili muwasikilize wananchi hawa n...
Marato tv - Sauti ya Jamii