Skip to main content

Posts

Showing posts from July 1, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WATUMISHI WEZI NA WAZEMBE KUKIONA CHA MOTO-MKUU WA MKOA KAGERA

  Na Angela Sebastian ;Bukoba  Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Yahya Ramadhan Kido amewataka  viongozi na,watumishi na wataalam wa mkoa huo kuhakikisha wanasimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi,weledi,uadilifu na kuzingatia taratibu zote za manunuzi na utaratibu wa mikataba ya inayohusu miradi husika ili raslimali za Umma zitumike kwa ufanisi. Kanali Kido ametoa maagizo hayo wakati wa warsha maalum iliyoandaliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU)Mkoa wa Kagera ya kuwajengea uwezo wadau kutoka sekta mbalimbali mkoani humo, juu ya usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambapo amesema katika miradi yote inapaswa kuzingatiwa ubora,muda wa utekelezaji,matumizi sahii ya fedha za Umma na kuhakikisha sheria zinafuatwa kikamilifu. Aidha amewataka wadau wanaohusika na usimamizi na utekelezaji wa miradi ya mbalimbali ya ujenzi kuhakikisha wanafanya upimaji wa vifaa wanavyotumia katika ujenzi wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, sambam...

SERENGETI YAOMBA UTEKELEZAJI WA HARAKA WA MIRADI YA MAJI, BARABARA NA UWANJA WA NDEGE

 Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Surati, ameiomba Serikali kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo barabara, maji na ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Serengeti ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na sekta ya utalii. Akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Serengeti uliofanyika leo Julai 1, 2026 mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Surati amesema wananchi wa eneo hilo wameendelea kuwa nguzo muhimu katika kulinda na kuhifadhi Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Ameeleza kuwa hifadhi hiyo ni miongoni mwa hazina kubwa za taifa, ikichangia kwa kiasi kikubwa mapato ya fedha za kigeni na mapato ya serikali, hivyo kuiweka Serengeti katika nafasi ya kipekee kimataifa katika sekta ya utalii. Aidha, ameshukuru Serikali kwa kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo mradi wa maji unaoendelea, huku akiomba ukamilishwe kwa haraka ili kutatua changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ambapo ameomba wananchi wa Serengeti kupat...

UCHUMI WA BULUU NI MLANGO MPYA WA UTAJIRI WA TAIFA

 …….Unahusisha uvuvi, usafirishaji, utalii, gesi, petrol na umwagiliaji. Na Mwandishi Wetu UTEKELEZWAJI wa sera ya uchumi wa buluu umetajwa kuwa lango kuu la uchumi kutokana na fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye sekta hiyo. Sekta ya uchumi wa buluu inahusisha mambo sita ambayo ni uvuvi, usafirishaji, utalii, gesi, petrol na umwagiliaji. Hayo yalisemwa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Uchumi wa Buluu na Uratibu Ofisi ya Makamu wa Rais, Magdalena Ngotolainyo, wakati akizungumzia uchumi wa buluu. Alisema Tanzania ni nchi iliyobarikiwa si kwa ardhi yenye rutuba pekee, wala si kwa madini, wanyamapori na vivutio vya utalii pekee, bali pia kwa utajiri mkubwa uliomo ndani ya maji yake. Bahari, maziwa, mito, mabwawa, maeneo oevu, maji chini ya ardhi na ukanda mpana wa pwani ni hazina ya kipekee ambayo, ikitumika kwa maarifa na uendelevu, inaweza kuwa injini mpya ya mageuzi ya kiuchumi na ustawi wa wananchi. Hii ndiyo nguvu ya Uchumi wa Buluu. Alisema uchumi wa buluu unahusisha ...

WAZIRI MKUU: HALMASHAURI KUTENGA ASILIMIA TANO YA MAPATO YA NDANI KUJENGA MIUNDOMBINU YA BIASHARA

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imeelekeza halmashauri zote nchini kutenga asilimia tano ya mapato yao ya ndani kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya biashara ili kuwawezesha wananchi, hususan vijana na wanawake, kufanya shughuli za kiuchumi katika mazingira bora na yenye tija. Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Ingwe Sekondari, Jimbo la Tarime Vijijini, wilayani Tarime, mkoani Mara, leo Jumatano, Julai 1, 2026, Waziri Mkuu alisema hatua hiyo inalenga kuondoa changamoto za maeneo ya biashara na kuongeza fursa za uzalishaji na ajira.  "Tumeenda kuweka asilimia tano kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maeneo ya biashara. Na kwenye hiyo asilimia tano, nimewaelekeza wenzetu wa TAMISEMI kwamba kama kuna eneo vijana wanalitaka kwa ajili ya kufanyia biashara, hata kama hilo eneo lina wamiliki, tumieni asilimia tano kulinunua. Msiwapeleke vijana kufanyia biashara maeneo ya mbali ambayo hayaendani na biashara wana...

DKT. NYANSAHO AWAHIMIZA WANANCHI WA SERENGETI KULINDA AMANI, AAHIDI KUFUATILIA KERO ZAO

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dkt. Rhimo Nyansaho, amewataka wananchi wa Wilaya ya Serengeti na Mkoa wa Mara kwa ujumla kuendelea kuwa nguzo ya amani na mshikamano, akisisitiza kuwa ulinzi na usalama wa taifa ni jukumu la kila Mtanzania bila kujali itikadi za kisiasa, dini au kabila. Dkt. Nyansaho ametoa wito huo leo Julai 1,2026 wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Serengeti, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, mkoani Mara yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Serikali ya Awamu ya Sita pamoja na kusikiliza kero za wananchi. Akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza, Dkt. Nyansaho amesema amani ndiyo msingi wa maendeleo endelevu, akiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha nchi inaendelea kuwa tulivu na salama. “Usalama na amani ya nchi yetu havina chama, havina dini wala havina kabila. Kila mmoja ana wajibu wa kuhakikisha Tanzania in...

DKT. MWIGULU: SERIKALI KUONDOA USUMBUFU KWA WAFANYABIASHARA

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imeanza kuchukua hatua za kuondoa vitendo vinavyowakwamisha wananchi kufanya shughuli za uzalishaji na biashara, huku ikielekeza nguvu katika kuboresha elimu, kutatua migogoro ya ardhi na kuhakikisha fedha za maendeleo zinatumika kwa uadilifu. Dkt. Nchemba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Sokoine, wilayani Serengeti, mkoani Mara, leo Jumatano, Julai 1, 2026. Amesema Serikali haitaki kuona wafanyabiashara na wananchi wanaofanya kazi kwa halali wakinyanyaswa kwa kukamatwa mali zao bila sababu za msingi, ikiwemo kufungiwa akaunti za benki, kuchukuliwa fedha, pikipiki, baiskeli na vifaa vyao vya kazi.  Katika sekta ya usafiri,Dkt. Nchrmba amesisitiza kuwa Serikali imeelekeza vyombo vya dola kutokamata pikipiki na magari yanayotumika halali kama mitaji ya wananchi isipokuwa pale ambapo vyombo hivyo vitahusishwa moja kwa moja na uhali...

SERIKALI YATENGA BILIONI 38 KUPIMA VIJIJI VYOTE TANZANIA, YAAGIZA KLINIKI ZA ARDHI KILA KATA

  Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, ametangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia utoaji wa kiasi cha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kupima vijiji vyote nchini ili kumaliza migogoro ya ardhi. Mhe. Mmuya amebainisha hayo leo, Julai 1, 2026, katika viwanja vya Sokoni Mugumu wilaya ya Serengeti mkoani Mara, alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi, zikiwemo zile za sekta ya ardhi. Katika hatua ya haraka ya kusogeza huduma kwa wananchi, Mhe. Mmuya amemuagiza Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Mkoa wa Mara pamoja na timu yake, kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha kliniki za ardhi katika kila kata na kila wilaya ya mkoa huo. "Hakikisheni mnaratibu uwepo wa kliniki za ardhi katika kila kata, kila wilaya ili muwasikilize wananchi hawa n...

MLIPUKO WA BARUTI WAUA MMOJA,WAJERUHI SABA NYAMAGANA

Na Dawati la Habari Polisi; Mwanza. Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine saba wakijeruhiwa kufuatia mlipuko wa baruti uliotokea leo Julai 1, 2026, majira ya saa 12:46 asubuhi katika kibanda cha kahawa kilichopo Mtaa wa Sahwa ya Juu, Kata ya Lwanhima, Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa, amesema aliyefariki ni Marco Msenyere (52), mpasua mawe na mkazi wa Semba-Lwanhima. Amesema marehemu alikuwa amefika katika kibanda hicho kunywa kahawa akiwa na begi dogo lililokuwa na baruti. Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mlipuko huo ulisababishwa na uzembe wa utunzaji wa baruti, baada ya marehemu kuweka begi lenye baruti karibu na jiko la mkaa lililokuwa linawaka. Joto kutoka kwenye jiko hilo lilisababisha baruti kulipuka. Majeruhi wa tukio hilo ni Daudi Joseph Baraka (54), Emmanuel Luhangwa Joseph (40), Yusufu Rajabu Nasoro (20), Zawadi Saimon Ndukeji (27), James Husse...