Skip to main content

Posts

Showing posts from July 31, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Akutana na Rais wa Afrexim bank

*_Aibua maeneo ya uwekezaji, ushirikiano zaidi na Tanzania_* WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya mazungumzo na Rais Mteule na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Biashara ya Afrika (Afreximbank), Dkt. George Elombi na kuainisha maeneo zaidi ya uwekezaji nchini Tanzania. Mheshimiwa Majaliwa amesema anaamini kuwa katika kipindi cha uongozi wa Dkt. Elombi, benki hiyo itaongeza kwa kiwango kikubwa mchango wake katika kusukuma mbele biashara, maendeleo ya viwanda na uwekezaji wa kimkakati barani Afrika ikiwemo Tanzania. “Tunapenda kukuhakikishia kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea kujitolea kikamilifu katika ushirikiano wake wa kimkakati na Afreximbank,” alisema. Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Majaliwa alihimiza umuhimu wa Afreximbank kukamilisha mpango wake wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha tiba nchini Tanzania (African Medical Centre of Excellence) ambacho kitakuwa na uwezo wa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi na pia kupunguza utegemezi wa rufaa za nje ya...

TADB yabeba maonyesho ya nane nane kwa milioni 400

Na Mwandishi Wetu, Dodoma BENKI ya Maendeleo ya Kilimo (TADB),imemshukuru Rais Samia Sulunu Hassan kwa kuipa fedha nyingi ambazo zimeiwezesha kuwakopesha wakulima wengi na hatimaye kutangazwa kuwa mionghoni mwa benki kubwa nchini Benki hiyo ndiyo  imekuwa Mdhamini Mkuu wa maonyesho ya wakulima  ya nane nane yanayoanza kesho Ijumaa kwenye viwanja vya nane nane mkoani Dodoma ambapo Makamu wa Rais Dk Philip Mpango anatarajiwa kuyatembelea. Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege wakati akizungumza na waandishi wa habari ,kuhusu maonyesho hayo na udhamini wa milioni 400 wa benki hiyo kwenye maonyesho hayo. Alisema TADB imeamua kudhamini maonyesho  hayo kama sehemu ya shamra shamra za kusherehekea miaka 10 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2015 na mafanikio makubwa waliyoyapata. Alisema TADB imefanya mambo makubwa kwenye sekta ya kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na sekta mbalimbali za serikali. Alisema benki hiyo ime...