Skip to main content

Posts

Showing posts from November 20, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Msama Awavaa Gen-z na Viongozi Wa Dini

 Msama: * Atoa kauli nzito akiwasihi GEN-Z, viongozi wa dini *Ampongeza Rais Samia kwa kuunda tume huru kuchunguza matukio ya Oktoba 29 MKURUGENZI wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama amesema kilichotokea Oktoba 29, kisijirudie na watanzania wote tuseme inatosha kwani sio utamaduni wetu Msama amesema hayo leo wakati akitoa maoni yake kuhusu tume iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuchunguza matukio ya vurugu za Oktoba 29, siku ya uchaguzi mkuu mwaka huu. Tume hiyo inayoogozwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Othoman Chande, ilizinduliwa na Rais Samia, katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, mjini Dodoma. Vurugu hizo ambazo hadi leo lengo lake hazijulikani, zimesababisha vifo, uharibifu wa miundombinu, mali za Serikali na watu binafsi .  Msama ambaye alikuwa mgombea Ubunge jimbo la Ukonga (CCM), alisema huu sio muda wa kunyoshena kidole kwamba nani alikosea na nani alikuwa sahihi bali ni wakati wa kutafakari na kusema imetosha. Kwa mujibu wa Msama, Rais Samia anastaili pon...

Kampeni ya majilo ya kupikia yapamba moto

📌 *Majiko 1,583 kuuzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku* . 📌 *Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya Tsh 11,200* . 📍 *HANANG*  Mkuu wa wilaya ya Hanang Mheshimiwa Almishi Hazali ametoa wito kwa wananchi wa wilaya ya Hanang kujitokezo kwa wingi  kununua majiko banifu ambayo yameanzwa kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku. Wito huo umetolewa leo tarehe 20 Novemba, 2025 na Mheshimiwa Hazali alipofika katika Tarafa ya Katesh Kata ya Nangwa kijiji cha Nangwa kukagua na kufatilia utekelezaji wa mradi ambapo jumla majiko 1,583 yatasambzwa  na kuuzwa kwa bei ya ruzuku wilaya nzima. “Mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni mwendelezo wa  juhudi za serikali  katika kutunza mazingira na kuboresha afya za  wananchi kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya kutosha ya umuhimu wa matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia” Alisema Mhe. Hazali. Akizungumza wakati wa uuzaji wa majiko hayo, msimamizi wa mradi kutoka REA, Ndugu Abdulrazack Mkomi...

Makamu Wa Rais Ashiriki Uwekaji Jiwe la Msingi la Ukarabati Mkubwa Wa Reli ya Tazara

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema ukarabati wa reli ya TAZARA utaimarisha Ukanda wa Kati na Kusini, kuchochea biashara Tanzania, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Bara la Afrika kwa ujumla. Makamu wa Rais amesema hayo wakati alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la uzinduzi wa Ukarabati Mkubwa wa Reli ya TAZARA iliyofanyika Jijini Lusaka nchini Zambia. Ameongeza kwamba ukarabati huo, utaongeza mauzo ya bidhaa nje na ndani ya Mataifa ya Zambia na Tanzania, kukuza kilimo, madini, viwanda, utalii na kutengeza ajira zaidi kwa wananchi wa ukanda huo. Makamu wa Rais amesema wakati reli ya TAZARA inaimarishwa, Tanzania inafanya maboresho ya kisasa ya bandari ikiwemo dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam kwa magati mapya, kuboresha ufanisi, n...

Dkt. Kijaji Apokea Rasmi Ofisi Wizara ya Maliasili na Utalii

Na Sixmund Begashe - Dodoma Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amekabidhiwa rasmi ofisi na mtangulizi wake Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) tayari kwa kuiongoza Wizara hiyo yenye mchango mkubwa kiuchumi nchini.  Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma leo Novemba 20,2025, Mhe. Dkt. Kijaji licha ya kumpongeza mtangulizi wake kwa hatua hiyo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumwamini na kumteua kwenye nafasi hiyo, huku akiahidi kuwatumikia vyema nafasi hiyo kwa maslahi mapana ya wananchi na  Taifa kwa ujumla. Aidha aliekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana(Mb), amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumwamini katika ngazi mbalimbali alizozitumikia na ameahidi kutoa ushirikiano kwa uongozi mpya wa Wizara hiyo pale itakapo hitajika. Zoezi hilo la Makabidhiano limeshuhudiwa  na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad  Has...

Dkt. Mwigulu Akutana na Katibu Mkuu wa TEC

Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Novemba 20, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima, katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam. 

WAZIRI MCHENGERWA AKABIDHIWA OFISI NA MHE. JENISTA MHAGAMA

Na WAF,  Dodoma Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Novemba 19, 2025 amekabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama. Tukio la makabidhiano ya ofisi limefanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya Mtumba, Jijini Dodoma. Waziri Mchengerwa amempongeza Mhe. Mhagama kwa utumishi wake hodari katika Wizara mbalimbali nchini ikiwemo Wizara ya Afya ambapo amefanya kazi kubwa ya kuboresha Sekta hiyo na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini. “Mhe. Rais ameahidi ndani ya siku 100 atafanya mageuzi makubwa ya Sekta ya Afya nchini, nashukuru kwa hatua nzuri ambayo ulishaanza utekelezaji wake ikiwemo suala la Bima ya Afya kwa wote pamoja na mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza nchini, ambayo yanaleta athari kubwa ndani ya jamii,” amesema Waziri Mchengerwa. Mhe. Mchengerwa amemtakia kila la heri Mhe. Mhagama na kuahidi kuendelea kushirikiana kwani  Wizara ya Afya ni mhimili mkubwa katika usalama wa nchi, hivyo watajitahidi kuhakikisha ndoto za M...

Waziri Ndejembi Akabidhiwa Ofisi na Aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Biteko

  Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi leo 20 Novemba, 2025 amekabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko kwenye ofisi za Wizara zilizoko mtumba mkoani Dodoma, na kumshukuru Mhe. Biteko kwa utendaji wake wa kazi katika kipindi chote cha uongozi wake. Waziri Ndejembi amesema katika kipindi cha uongozi wake, utendaji kwenye sekta ya nishati umekuwa kwa kiasi kikubwa na huduma za utendaji zimeboreshwa na tija kuonekana katika harakati za kukuza sekta ya nishati. Waziri Ndejembi ameahidi atayaendeleza yote pale alipoishia Mhe.Biteko, ili kuhakikisha azma ya serikali na maono iliyonayo kufanikisha miradi ifikapo 2030 yanafikiwa. Kwa upande wake, Mhe. Dkt. Biteko amempongeza Mhe. Deogratius Ndejembi kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na kumhakikishia kumpa ushirikiano wakati wowote katika kufanikisha maono makubwa ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Sekta y...

Tume Yasisitiza Elimu ya Local Content na Utekelezaji wa Csr

  _Ajira za Migodini Zafikia 19,874, Watanzania Wafanya Kazi kwa Asilimia 97.5_ DODOMA  Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, ametoa wito kwa Waratibu wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini (Local Content) na CSR katika mikoa kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa wananchi ili kuhakikisha Watanzania wananufaika ipasavyo na rasilimali za madini. Akizungumza leo Novemba 20, 2025 jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo kwa waratibu hao, Mhandisi Lwamo amesema ni muhimu kusimamia kwa umakini Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini pamoja na Wajibu wa Wamiliki wa Leseni kwa Jamii (CSR) ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa madini na sekta nyingine zinazohusiana. “Elimu kwa wananchi ni nguzo muhimu ya kuwawezesha kuchangamkia fursa za ajira na biashara migodini, hususan baada ya Tume kutangaza orodha ya bidhaa na huduma zinazopaswa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa na W...