MWaziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema Mkoa wa Mbeya na kwa ujumla Nyanda za Juu Kusini una uwezo mkubwa wa kuongeza mchango wake katika uchumi wa Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kuongeza uzalishaji, kuchakata mazao na kuimarisha uwekezaji katika viwanda. Mhe. Balozi Omar ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja mkoani Mbeya, ambapo alitembelea Ofisi za Mkoa za Chama cha Mapinduzi (CCM), jijini Mbeya. Amesema Nyanda za Juu Kusini zinachukua takribani asilimia 20 ya eneo lote la Tanzania, lakini mchango wake katika Pato la Taifa bado haujaakisi kikamilifu ukubwa wa eneo hilo na utajiri wa fursa zilizopo. Amesema hali hiyo inatoa nafasi kwa Serikali, sekta binafsi na wadau wengine kuongeza uwekezaji katika kilimo, madini, viwanda na sekta nyingine za uzalishaji ili kuongeza tija na mapato ya wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla. “Bado tuna fursa kubwa sana ya kuimarisha mchango wetu katika pato la Taifa uendane na eneo tulilonalo, na si kwa s...
Marato tv - Sauti ya Jamii