Skip to main content

Posts

Showing posts from June 6, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WASIRA:UJAMAA BADO NI MSINGI WA MAENDELEO NCHI

*Elimu bila malipo, Bima ya Afya kwa Wote ni ushindi* MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, Stephen Wasira, amesema ujamaa bado ni msingi mkuu unaoendesha sera na mipango ya maendeleo nchini. Akizungumza na wanachama wa CCM mjini Moshi, leo Juni 6 2026, Wasira alisema alikana madai kuwa mfumo huo umepitwa na wakati. "Wale wanaojidanganya hawaujui. Misingi inayoendesha nchi sasa ni ileile ya ujamaa. Tuanzie na elimu bila malipo, tuendelee na jitihada za kuanzisha Bima ya Afya kwa wote. Haya yote ni mafanikio ya ujamaa," alisema. Wasira alitoa mfano wa Mkoa wa Kilimanjaro, akibainisha kuwa kama sio ujamaa, ardhi na mashamba ya kahawa yangekuwa yamenunuliwa na watu binafsi na wananchi wasingeweza kumiliki. "Kama hapa Kilimanjaro tungekosa ujamaa, kahawa yote ingenunuliwa. Ni uongo kusema ingekuwa bado mikononi mwa wananchi," alieleza. Pia, alizungumzia umuhimu wa uwekezaji wa sekta binafsi, akisema ni jambo la kawaida na la lazima kwa ukuaji wa uchumi wa ...

DKT. MWIGULU AAGIZA UCHUNGUZI WA MAPATO YA MAEGESHO IFUNDA

  WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo la Ifunda wilayani Iringa na kuwasilisha taarifa kamili kuhusu namna mapato hayo yalivyokuwa yakikusanywa kabla na baada ya mabadiliko ya mfumo wa ukusanyaji pamoja na matumizi yake. Ametoa agizo hilo leo Jumamosi, Juni 6, 2026 wakati akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Jimbo la Kalenga katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ifunda wilayani Iringa mkoani Iringa. Agizo hilo lilitolewa baada ya Waziri Mkuu kuwataka viongozi wa TANROADS, Halmashauri na TAKUKURU kutoa maelezo kuhusu mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo hilo na mabadiliko yaliyofanyika katika usimamizi wake. “Nataka ripoti yote ya zoezi la ukusanyaji jinsi ambavyo limefanyika, kabla na sasa. Nataka tujue fedha hizi zimeenda wapi na wahusika walikuwa nani,” alisema Dkt. Mwigulu. Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kupitia mifumo...

TANZANIA YA KIJANI: MAAMUZI YA LEO, URITHI WA KESHO

 Na Gideon Gregory - Dodoma  Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kukabiliwa na ongezeko la joto, uchafuzi wa mazingira mjadala kuhusu mazingira haupo tena kwenye uhifadhi pekee bali umehamia kwenye namna ambavyo mataifa yanajenga maendeleo yanayodumu.  Takwimu za Umoja wa Mataifa za miaka ya hivi karibuni zinaonyesha kuwa shinikizo la mazingira linaongezeka kila mwaka na kufanya hatua za sasa kuwa msingi wa maisha ya vizazi vijavyo. Ni katika muktadha huo ambapo maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu kwa Tanzania yamekuja na ujumbe wa “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania” kauli inayobeba zaidi ya kampeni ya kupanda miti ili kurejesha uoto wa asili. Akizungumza kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyila Jijini Dodoma Mei 5,2026 Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi anabainisha kuwa mazingira yanamchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa na ustawi wa wananchi.  "Pale ambapo mazingira yametunzwa vyema basi uchumi na ustawi wa maisha ya wa...