Skip to main content

Posts

Showing posts from June 6, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

HOTUBA YA RAIS SAMIA URUSI NI USHINDI KIUCHUMI, KIJAMII, NA KIDIPLOMASIA!

Na Beda Msimbe,TBN, aliyekuwa Urusi IJUMAA Juni 5, 2026 ilikuwa siku ya kihistoria na ya kipekee, wakati Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alisipomama mbele ya viongozi wa dunia katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi (St. Petersburg International Economic Forum) na hoja nzito zenye mashiko, akibeba sauti ya Watanzania wote na kuweka wazi fursa zinazopatyikana Tanzania ikiwa na pamoja na mwelekeo mpya wa nchi katika kutengeneza uchumi wa kisasa. Jukwaa hilo lilikuwa sehemu muhimu ya ziara ya Rais Samia ambayo haikuwa tu ya itifaki, bali ya kueleza milango wazi ya fursa za kiuchumi na kijamii. Jinsi Rais Samia alivyopokewa na kukirimiwa nchini Urusi katika shughuli zoye zilizomhusu, ilionesha taswira ya urafiki wa dhati na cheko tupu kati yake na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin. Ziara hiyo ilirudisha historia, ikaweka wazi haja ya sasa baada ya ukombozi wa kisiasa kusaidiana kupatikana kwa ukombozi wa kiuchumi na ustawi wa jamii zote mbili. Akiwa katika jukwaa la kiuchumi, akizungu...

CHADEMA YAJIFUNGIA ZANZIBAR KUWEKA MIKAKATI YA KISIASA

Leo, tarehe 07 Juni 2026, Kamati Maalum ya CHADEMA Zanzibar imeketi katika kikao chake kilichofanyika Kisiwani Pemba. Kikao hicho kimeongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Mhe. Said Mzee Said, na kuhudhuriwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Mhe. John Heche, pamoja na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Mhe. John Mnyika. Kikao hicho kinajikita katika kujadili hali ya siasa ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla, kwa lengo la kufanya tathmini ya mwenendo wa kisiasa na kuweka mwelekeo wa hatua za chama katika kipindi kijacho. Aidha, kikao hicho kinajadili na kupitisha Mpango Mkakati wa CHADEMA Zanzibar wa miaka mitano, utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa shughuli, sera na vipaumbele vya chama kwa kipindi husika.

WANU ATAKA USHIRIKIANO KATI YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI KUTATUA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA

  Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na taasisi za elimu katika kuwaandaa vijana kwa soko la ajira kupitia mafunzo yanayozingatia mahitaji halisi ya sasa. Mhe. Wanu ametoa rai hiyo Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake katika Kiwanda cha Superdoll, ambapo amehimiza utoaji wa elimu inayojikita katika ujuzi na umahiri ili kuwajengea wahitimu uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kuendana na mahitaji ya sekta za uzalishaji. Mhe. Ameir ameeleza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa vyuo 65 vya VETA na kuboresha vingine 12, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa mafunzo ya ufundi stadi na kuwawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika uchumi unaobadilika.  Mhe. Wanu ameendelea kuzihimiza taasisi na wadau wengine kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kufungua milango ya mafunzo ya vitendo kwa vijana na wakufunzi ili kupunguza pengo kati ya maarifa ya d...

SAMIA ATANGAZA UTALII ALIPANIA SOKO LA URUSI

 Na Beda Msimbe,TBN, Petersburg, Urusi Ushirikiano wa miaka 65 ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi sasa unatafsiriwa kuwa daraja imara la maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku sekta ya utalii ikichukua mwelekeo mpya wa kimkakati kuvutia masoko ya kimataifa likiwemo la Urusi.  Alisema anatambua soko la Urusi ni kubwa naTanzania ipo tayari kulihudumia kwa kuondoa vikwazo kadhaa ikiwamo kuwezesha kupatikana kwa safari za moja kwa moja kutoka Moscow hadi Dar es Salaam na Zanzibar. Rais alisema hayo wakati akihutubia wawakilishi kutoka nchi 130 duniani zilizoshiriki mkutano wa kiuchumi wa kimkataifa wa Petersburg Juni 5, 2026. Katika jukwaa hilo la kiuchumi, Rais Samia alitangaza kuwa kuanzia Julai 2 mwaka huu, Shirika la Ndege la Tanzania, Air Tanzania, litaanza safari za moja kwa moja kati ya Dar es Salaam, Moscow, na Zanzibar kwa lengo la kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia laki tano ifikapo mwaka 2030 na hatimaye milioni moja.  Hatua hii inaenda sambamba na ush...

TANZANIA IKO TAYARI KWA BIASHARA, UWEKEZAJI NA UBUNIFU

 Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi Katika hotuba ya kihistoria iliyotolewa kwenye Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg nchini Urusi, Rais wa Tanzania amewahakikishia viongozi wa dunia na wawekezaji wa kimataifa kuwa nchi hiyo iko tayari kwa biashara, uwekezaji mkubwa, na ubunifu wa kisasa ili kuendana na ushindani wa soko la kimataifa.  Rais Samia akihutubia Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Saint PeterburgTanzania imefanya mageuzi makubwa ya kisheria na kitaasisi ikiwemo kuanzisha kituo kimoja cha huduma ambapo usajili wa kampuni sasa huchukua hadi saa 24 tu. Alisema hatua hiyo imechangia kupaa kwa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje hadi kufikia dola bilioni 12 mwaka 2025 ikilinganishwa na dola bilioni 3 tu za mwaka 2021.  Ili kuchochea ukuaji huu wa viwanda na biashara, aliwaambia washiriki wa jukwaa hilo kutoka nchi takribani 130 kwamba serikali imeweka msisitizo mkubwa katika usindikaji wa madini ya mkakati ndani ya nchi kama vile dhahabu, neli, grap...

PUTIN AIKUBALI TANZANIA AELEZA JINSI ILIVYO MUHIMU

 Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema Tanzania ni lango kuu la kimkakati linalounganisha soko la Afrika Mashariki na masoko ya kimataifa. Aidha amesema katika uchumi wa dunia unaozidi kubadilika kuelekea mifumo ya nguzo nyingi za kiuchumi, taifa la Tanzania umuhimu mkubwa katika kuyfanikisha ustawi wa jamii mbalimbalio.  Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg la mwaka 2026 Rais Putin amesema kuwa Tanzania katika utendaji ni taifa la kimkakati katika ukanda wa Afrika Mashariki unaofanana na ule wa nchi ya Uzbekistan katika ukanda wa Asia ya Kati ikifanya kazi kama kiungo muhimu sana kati ya uchumi wa kikanda na vituo vikuu vya biashara ya kimataifa duniani.  Kiongozi huyo amebainisha hayo wakati akizungumzia mataifa ambayo kutokana na nafasi zao za kijiografia na mahusiano yao ya kiuchumi yanageuka kuwa madaraja muhimu kati ya kanda tofauti duniani na kuongeza kuwa mataifa yenye uwezo wa kuoanisha maendel...

WASIRA:UJAMAA BADO NI MSINGI WA MAENDELEO NCHI

*Elimu bila malipo, Bima ya Afya kwa Wote ni ushindi* MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, Stephen Wasira, amesema ujamaa bado ni msingi mkuu unaoendesha sera na mipango ya maendeleo nchini. Akizungumza na wanachama wa CCM mjini Moshi, leo Juni 6 2026, Wasira alisema alikana madai kuwa mfumo huo umepitwa na wakati. "Wale wanaojidanganya hawaujui. Misingi inayoendesha nchi sasa ni ileile ya ujamaa. Tuanzie na elimu bila malipo, tuendelee na jitihada za kuanzisha Bima ya Afya kwa wote. Haya yote ni mafanikio ya ujamaa," alisema. Wasira alitoa mfano wa Mkoa wa Kilimanjaro, akibainisha kuwa kama sio ujamaa, ardhi na mashamba ya kahawa yangekuwa yamenunuliwa na watu binafsi na wananchi wasingeweza kumiliki. "Kama hapa Kilimanjaro tungekosa ujamaa, kahawa yote ingenunuliwa. Ni uongo kusema ingekuwa bado mikononi mwa wananchi," alieleza. Pia, alizungumzia umuhimu wa uwekezaji wa sekta binafsi, akisema ni jambo la kawaida na la lazima kwa ukuaji wa uchumi wa ...

DKT. MWIGULU AAGIZA UCHUNGUZI WA MAPATO YA MAEGESHO IFUNDA

  WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo la Ifunda wilayani Iringa na kuwasilisha taarifa kamili kuhusu namna mapato hayo yalivyokuwa yakikusanywa kabla na baada ya mabadiliko ya mfumo wa ukusanyaji pamoja na matumizi yake. Ametoa agizo hilo leo Jumamosi, Juni 6, 2026 wakati akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Jimbo la Kalenga katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ifunda wilayani Iringa mkoani Iringa. Agizo hilo lilitolewa baada ya Waziri Mkuu kuwataka viongozi wa TANROADS, Halmashauri na TAKUKURU kutoa maelezo kuhusu mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya maegesho katika eneo hilo na mabadiliko yaliyofanyika katika usimamizi wake. “Nataka ripoti yote ya zoezi la ukusanyaji jinsi ambavyo limefanyika, kabla na sasa. Nataka tujue fedha hizi zimeenda wapi na wahusika walikuwa nani,” alisema Dkt. Mwigulu. Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kupitia mifumo...