#Awataka kukamilisha kazi kwa wakati Dar es Salaam Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff amewataka makandarasi wanaotekeleza kazi za ukarabati na matengenezo ya barabara vivuko na madaraja katika maeneo yaliyoharibiwa na mvua za El nino nchini kutekeleza mikataba yao kwa wakati huku wakizingatia masuala ya msingi ikiwemo usalama mahali pa kazi pamoja na utunzaji wa mazingira. Mhandisi Seff ameyasema hayo wakati wa kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam kati ya TARURA na Makandarasi hao wanaotekeleza miradi hiyo nchi nzima. “Hakikisheni katika utekelezaji wa miradi yote mnakamilisha kwa wakati pia mnazingatia masuala yote ya usalama na mazingira kama ilivyoainishwa kwenye makubaliano ya jumla ya miradi hii”Alisisitiza. Naye, Mratibu wa miradi ya Benki ya Dunia kutoka TARURA Mhandisi Humphrey Kanyenye amesema kwamba wao kama waratibu wa miradi hiyo wapo tayari kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kila mkand...
Marato tv - Sauti ya Jamii