Skip to main content

Posts

Showing posts from September 30, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Dkt.Mwinyi:Smz inaendelea kuifungua pemba

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameizindua meli ya kwanza ya makontena katika Bandari ya Mkoani na kuwataka wafanyabiashara kutumia fursa hiyo kuifungua Pemba kiuchumi. Rais Dk. Mwinyi ameshuhudia meli ya Lamu Shipping Limited ikishusha kwa mara ya kwanza makontena kwenye Bandari ya Mkoani, hatua aliyoielezea kuwa ni mapinduzi makubwa kwa sekta ya usafirishaji hapa nchini. Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 30 Septemba 2024, alipozungumza na wananchi katika eneo la Bandari Kavu ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba. Pia, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa kinachofanywa na Serikali si kuzikodisha bandari bali ni kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza tija na ufanisi katika uendeshaji wa majukumu ya bandari zote nchini. Aidha, amefahamisha kuwa hatua ya kuanza kushushwa kwa makontena kwenye bandari hiyo itarahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji na kuwaondolea wafanyabiashara mzigo wa gharama kubwa. Rais Dk. Mwinyi amewahakikishia wa...

Biteko ahimiza utatu wa mzazi,mwalimu na mwanafunzi

 Na Mwandishi Wetu, MUHEZA NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mh Dk Doto Biteko, amehimiza jamii kudumisha ushirikiano na mahusiano mema kati ya mzazi, mwalimu na mwanafunzi, ili kumjenga mtoto katika ubora wa maisha yake na taaifa kwa ujumla. Mhe Dk Biteko ameyasema hayo leo Septemba 30, 2024 alipokuwa akizindua kampeni ya Mtoto wa Leo Samia Kesho, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Juma la Elimu katika wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Amesema ushirikiano na mahusiano hayo ni nyenzo muhimu ya kujenga mazingira bora kwa mtoto kuanzia ngazi ya familia, kwenye jumuiya za watu na shuleni anapopata elimu na maarifa ya kumfanya (mtoto) kuwa mwenye manufaa na tija katika ngazi zote. Mhe Dk Biteko, amewaelekeza walimu kumtazama mtoto kama kiongozi, mhandisi, daktari, mwanataaluma, kiongozi ama mzazi bora wa baadaye, na hivyo kumlinda, kumpa elimu, ujuzi, maarifa na kumlinda dhidi ya dhuluma zinazomkabili. Pia amewaasa wazazi na walezi kuepuka matumizi majina na maneno yasiyofaa kwa watoto,...

Waziri mkuu afanya mazungumzo na mkurugenzi mtendaji wa Amref

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Septemba 29, 2024 alifanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Amref Health Africa Dkt. Githinji Gitahi, kando ya Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA 79) ambao alishiriki kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  Jijini New York,  Katika mazungumzo hayo Mheshimiwa Majaliwa alilipongeza shirika hilo kwa kazi kubwa inayofanya kwenye sekta ya afya nchini Tanzania na alimuahidi Mkurugenzi Mtendaji huyo kuwa Serikali itaendelea kuwapa ushirikiano ili mipango na malengo ya shirika hilo ya kuisaidia  sekta ya nchini yaendelee kufanikiwa. Amesema kuwa jitihada ambazo shirika hilo limekuwa likizifanya kwenya sekta ya afya nchini Tanzania zimeendelea kuzaa matunda na kuwezesha kuwafikia watanzania wengi kwenye huduma ya afya “Kwenye hili niendelee kukuomba uamini kwamba Tanzania ni rafiki wa kweli kwenye mipango ya Shirika, mafanikio ya kupunguza vifo vya mama na mtoto yanatokana na mahusiano y...

Bashe awaonya wafanyabiashara watakaobainika kuhujumu ununuzi wa korosho

  Na NIRC, Mtwara WAZIRI wa Kilimo Hussein Bashe amesema hatasita kuendelea kuwafutia leseni wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanaotumika na waleta janja janja katika ununuzi wa korosho na kunyonya wakulima. Amesema hatua ya Serikali kuwapa kipaumbele wafanyabiashara wa ndani kununua korosho moja kwa moja kwa wakulima haikulenga kufungua mianya ya unyonyaji. Akizungumza katika muendelezo wa ziara yake mkoani Mtwara ,Waziri Bashe amesema amefanya ziara hiyo mapema kabla ya msimu kuanza ili kusiwepo na kutoelewana. Amesema anatambua wanaosemea wakulima si wakulima, hivyo hatasita kufuta leseni ya biashara kwa wafanyabiashara wakubwa, wadogo, wakati na wenye viwanda wanaofanya ujanja ujanja na kunyonya wakulima. Ameongeza kuwa, muhimu ni kila mmoja kufuata bei elekezi kwa kuwezesha sekta ya kilimo cha korosho kupiga hatua. “Kuna mtu ana hangaika kuanzia Oktoba kwa mwaka mzima, anaenda mnadani kipato chake ni kimoja kwa mwaka halafu kuna mtu yupo katikati, anafanya ujanja ujanja wa ku...

Rais Samia akiwa katika matukio mbalimbali wakati wa kuzindua kitabu cha maisha ya Edward Sokoine

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na wake wa hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya kuzindua Kitabu kinachohusu Maisha na Uongozi wake katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 30 Septemba, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uzinduzi wa Kitabu cha Hayati Edward Moringe Sokoine kinachohusu Maisha na Uongozi wake katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 30 Septemba, 2024. Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi waliohudhuria hafla ya Uzinduzi wa Kitabu cha Hayati Edward Moringe Sokoine kinachohusu Maisha na Uongozi wake katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 30 Septemba, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Mtoto wa hayati Edward Moringe Sokoine, Balozi Joseph Edw...