Skip to main content

Posts

Showing posts from February 15, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Dk. Mwinyi Apokewa Kwa Kishindo Pemba

*#Wanachama 2,439 wa ACT wajiunga na CCM* Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Hussein Ali Mwinyi  amezisisitiza Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi kuwahamasisha Wanachama na Wananchi kujiandikisha na kujitokeza kwa Wingi kupiga Kura ili CCM ishinde kwa Kishindo. Dkt. Mwinyi ambae ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya CCM ameyasema hayo alipozungumza  na Wanachama na Wananchi Mauwani, Kiwani Mkoa wa Kusini Pemba Katika Mkutano Maalum wa Mapokezi  yake baada ya Kuteuliwa hivi Karibuni kuwa Mgombea wa Urais wa Zanzibar. Dkt.Mwinyi amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya  Wana CCM kutojitokeza kupiga kura wakati wa Uchaguzi jambo linaloipunguzia Kura za Ushindi Chama hicho. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza UWT kwa kazi nzuri walioifanya ya Uhamasishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura na kuiagiza kuendelea na mwamko huo. Hali kadhalika Dkt.Mwinyi amewapongeza na  kuwakaribisha Wanachama 2,439 wa Chama cha ACT Wazalendo kwa Uamuzi wa Kujiunga na CCM...

Rais Wa Burkina Faso Amtembelea Baba Ake

Rais wa Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traore akiwa na Baba yake mzazi, alipokuwa amemtembelea shambani kwake.   

Majaliwa Mgeni Rasmi Mkutano Mkuu Jimbo La Maswa Mashariki

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu wa Ndugu Kassim Majaliwa leo Februari 16, 2025 ni mgeni rasmi kwenye Mkutano Mkuu Maalum Chama cha Mapinduzi Jimbo la Maswa Mashariki, mkoani Simiyu.

Zoezi la Kijeshi kati ya Jwtz na Jeshi la Marekani lafungwa

  Zoezi hilo hilo linalojulikana Justifed Accord ambalo lilizinduliwa rasmi Februari 10 mwaka huu, ikiwa ni ushirikiano uliopo Katika ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la Marekani ili kujenga ushirikiano wa usalama kupitia mazoezi ya pamoja ya kijeshi. Akizungumza Leo, 15, Februali 2025, katika kituo cha mafunzo Cha jeshi la Msata Mkoani Pwani, wakati wa kufunga mazoezi hayo Meja Jenerali Selemani Mzee ambaye amemuwakilsha mkuu wa majeshi Nchini Jenerali John Mkunda, amesema kuwa mazoezi ya ushirikiano wa kawaida ambayo huwa wanayafanya na Nchi rafiki. Amesema mazoezi hayo ni kama sehemu ya ushirikiano endelevu wa kijeshi na usalama kati ya Tanzania na Marekani yamelenga kuboresha usalama wa Kanda na uwezo wa kulinda amani ambayo yatashirikisha vikosi vya ardhini vya Tanzania na Marekani ambayo yametoa uzoefu wa thamani Katika mbinu za kukabiliana na vifaa vya mlipuko vya kutengeneza,Ulinzi wa kijinsia, taratibu za uokoaji wa matibabu na ujumuishaji wa ndege zenye rubani ...

Rais Samia Azungumza Na Waziri Mkuu Wa Ethiopia

 Rais Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akutana na kuzungumza na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe. Abiy Ahmed kando ya Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia

Kwenye Urais Tumeishamaliza-Majaliwa

▪️Asisitiza Rais Dkt. Samia tunaye na tunaenda naye._ ▪️Asema Rais Samia ni mgombea aliyejipambanua kwa uhodari na uimara wake kiutendaji_ ▪️Amtaja Dkt. Nchimbi kuwa kiongozi mchapakazi na anatosha kwenye nafasi ya ugombea mwenza._ Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi kimeshamaliza mchakato wa kupata mgombea Urais wa Chama hicho katika uchaguzi Mkuu utakaofanya baadae mwaka huu wa 2025. Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi (Februari 15, 2025) wakati Mkutano Mkuu Maalum Chama cha Mapinduzi Jimbo la Itilima, uliofanyika katika uwanja wa Stand Mpya ya Itilima, mkoani Simiyu. Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi chama hicho kimewapa ridhaa ya kuendelea kuwatumikia Watanzania katika kipindi cha 2025-2030. “Mama yupo na sisi, tunaye na tunaenda nae, Mwaka huu tumewaleta wagombea bora kabisa ambao...

Wananchi Wa Kata Za Busambara Na Kiriba Musoma Vijijini Wamshukuru Rais Samia Kupata Maji Ya Bomba

Na Shomari Binda-Musoma  WANANCHI wa Kata za Busambara na Kiriba zilizopo jombo la Musoma vijijini wamemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kupata mradi wa maji ya bomba. Licha ya kumshukuru Rais Samia wamemshikuru pia mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Profess Sospeter Muhongo kwa ufatiliaji wake wa karibu na kufanikisha kufikiwa na maji safi na salama. Shukurani hizo wamezitoa kwa nyakati tofauti kwenye Kata hizo wakati wa zìara ya Kijiji kwa Kijiji inayofanywa na mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka. Wananchi wa Kata ya Busambara wamesema wameangaika kwa muda mrefu na sasa wameondokana na shida ya maji. Wamesema shida ya maji iliwafanya kushindwa kufanya shughuli nyingine za kiuchumi kwa wakati wakitafuta maji Mmoja wa wananchi hap aliyejitambulisha kwa jina la Mukama Mgeta amesema Rais Dkt.Samia ana deni kubwa kwao na malipo yake ni kumpa kura za kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa 2025. " Tunamshukuru sana Rais Dkt.Samia kwa mradi huu wa maji na sasa tunapata maji safi na ...