Skip to main content

Posts

Showing posts from January 16, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Uhalifu wadhibitiwa Visiwani, Viongozi wa Vijiji waonywa

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limeendelea kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika maeneo yote majini na nchi kavu kupitia doria na misako inayo endelea. Kupitia misako hiyo iliyofanyika siku mbili tarehe 15 na 16 mwezi huu zaidi ya watuhumiwa 30 wa makosa mbalimbali wamekamatwa katika visiwa vya Soswa, Chembaya, Chamagati na Nyamango katika Halmashauri ya Buchosa, wilaya ya Sengerema.  Akizungumza na wananchi wa Kisiwa cha Soswa Januari 16.2025 kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafugwa ameonya vikali baadhi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu katika maeneo ya visiwani wakiwemo baadhi ya viongozi wa vijiji wanaoshindwa kutoa ushirikiano na kuwaficha wahalifu katika maeneo yao. "Viongozi wa vijiji mnawajibu wa kusaidia kuundwa kwa vikundi vya ulinzi shirikishi ili kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyoanza kuchipuka kwenye maeneo yenu na sio kuwaficha wahalifu" ameonya kamanda Mutafugwa  Kamanda Mutafungwa, amesema kuwa oper...

Dc Chikoka aongoza Wananchi Kuchimba Msingi Ujenzi Shule Ya Kwanza ya Ghorofa

  Na Shomari Binda-Musoma MKUU wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka leo januari 17 amewaongoza wananchi kwenye nguvu kazi ya ujenzi wa shule ya kwanza ya gorofa. Shule hiyo inajengwa kwengwa kwenye Kata ya Kigera manispaa ya Musoma ikiwa na vyumba 8 vya madarasa. Akizungumza wakati wa zoezi hilo Chikoka amewashukuru wananchi waliojitokeza na kudai wameingia kwenye historia. Amesema shule hiyo itakapo kamilika watakuwa wameingia kwenye historia kubwa ambayo haitaweza kufutika. Chikoka amesema watahakikisha wanakamilisha msingi na kumuachia kazi mkandarasi aendelee na ujenzi. " Leo ni siku ya historia kwa wananchi wote mliojitokeza kwenye zoezi hili na kwa wingi wenu mmeonyesha utayari wa kupokea shule hii. " Ni Shule ya kwanza ya gorofa kwenye manispaa yetu ya Musoma na inaendelea kutupa heshima na kutoa nafasi kwa watoto wetu kusoma maeneo sahihi",amesema. Mkuu huyo wa Wilaya amemshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo ikiwemo ya elimu. Kwa up...

Rais Samia aongoza Kikao cha Kamati Kuu Ikulu Dodoma

  MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kinachoketi leo tarehe 17 Januari 2025, Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika tarehe 18 na 19 Januari, jijini Dodoma.

Uwanja wa Ndege Musoma Kuendelea na Ujenzi Wake Wiki Ijayo

  Na Shomari Binda-Musoma UJENZI wa upanuzi wa uwanja wa ndege Musoma unatarajiwa kuendelea wiki ijayo baada ya taratibu mbalimbali kukamilika. Hii imekuwa habari njema kwa wawekezajj wa biashara ya utalii wakiwemo wa hotel na watumiaji wengine wa uwanja huo. Akizungumza na Mwandishi wa Habari hii meneja wa TANROADS mkoa wa Mara mhandisi Vedastus Maribe amesema ujenzi huo utaendele na matarajio ni kwenda kwa kasi. Amesema yapo mambo ambayo yamekamilishwa na serikali ikiwa ni pamoja na malipo ya fidia kwa wananchi na kutoa nafasi ya kuendelea na ujenzi huo. Mhandisi Maribe ameishukuru serikali ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha na zikiwemo za fidia kwa wananchi ambao tayari wameanza kulipwa. Amesema wao kama wasimamizi watasimamia na kufatilia kwa weledi mkubwa ili kuona uwanja huo unakamilika. " Tutaendelea na ujenzi wiki ijayo na tunatoa shukrani kwa serikali yetu chini ya Dkt.Samia kuhakikisha tunaukamilisha ujenzi huo",amesema. Katika siku za hivi karibuni waw...

MISA Tanzania yawatembelea wadau wa habari, Kanda ya Ziwa

Mwandishi wetu ;Mwanza Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bwana Edwin Soko Leo amefanya ziara kwenye Taasisi za Kitaifa zenye Makao Makuu Kanda ya Ziwa zikiwemo Mamlaka ya Uthibiti wa  Nishati na Maji(EWURA) Kanda ya Ziwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) Kanda ya Ziwa. Soko amekutana na Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandishi Imelda Salumu  na kujadilili nama ya kufanya kazi Kwa pamoja likiwemo eneo la kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari kuelekea uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu ili wafanye kazi Kwa weledi zaidi. Kwa upande wake Mhandishi Imelda alieleza kuwa anaipongeza  MISA Tan Kwa kuona umuhimu wa kuwa karibu na wadau mbalimbali wa habari na  kusisitiza ataendelea kufanya kazi pamoja na wanachama wa MISA na waandishi wa habari wote nchini. Wakati huo huo Soko alikutana pia na Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa George Mhina ambapo walijadili juu ya umuhimu wa MISA  Tan kwenye kusimamia weledi ndani ya taaluma ya habari. Mhina alisema kuwa, EWURA wapo tayari kushirikian...