Skip to main content

Posts

Showing posts from December 3, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Sababu za Wananchi Kutotumia Mifumo Rasmi Kuwasilisha Malalamiko Serikalini Yatajwa

Na Hamida Ramadhan,  Dodoma Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala  Bora, Xavier Daudi amesema Wananchi walio wengi wamekuwa wakitumia mitandao ya Kijamii kufikisha malalamiko yao kwenye Taasisi za Serikali kutokana na  baadhi ya  Watumishi wa Umma kuvujisha siri za wateja wao pindi wananchi hao wanapotumia mifumo rasmi kutoa mrejesho Amesema vitendo hivyo vimekuwa vikiwakatisha tamaa Wananchi wenye nia njema ya kuona Serikali inakuwa kinara wa kutoa huduma bora kwa wananchi wake. Daudi ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo maalum ya siku tatu kwa Maafisa Mrejesho kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma  Amewataka Maafisa hao kutunza siri za wateja wao ili kuwafanya Wananchi kuwa huru kuwasilisha changamoto zinazowakabili  wakati wowote na mahali popote pasipo kulazimika kutumia mitandao ya kijamii Amesema kuwa, Mfumo wa e-Mrejesho unampa fursa  mwananchi  kut...

Mhe. Kapinga: Serikali Inakusudia Kupeleka Umeme Maeneo Yote ya Vijiji na Vitongoji

Na Mwandishi Wetu Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga, amesema umeme ni ajenda kubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayolenga kufikisha umeme kwenye maeneo yote ikiwemo vijiji na vitongoji. Amesema Serikali ipo kazini kuhakikisha ajenda hiyo inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa kupitia miradi mbalimbali ya umeme. Kapinga ameyaeleza hayo wakati alipotembelea Vitongoji vya Migwala na Oloodo Larkaria kata ya Sepeko wilayani Monduli mkoani Arusha tarehe 03 Disemba 2024,  Kapinga amewatoa wasiwasi wananchi kuhusu umeme kufika kwenye maeneo ambayo bado hayana umeme akisema  kuwa ili umeme ufike kwenye vitongoji ni lazima kwanza ufike kwenye vijiji vyote, ambapo vimesalia vijiji visivyozidi 70 nchini ili kukamilisha adhma ya Serikali kuhakikisha kila kijiji kinafikiwa na umeme. Aidha Naibu Waziri Kapinga amesema tayari vijiji vyote 368 vilivyopo katika mkoa wa Arusha vimepata umeme na vitongoji 981kati ya 1656 vimefikiwa na huduma hiyo. Akiwa kitongoji cha Oloodo Larkaria Kapinga a...

Majiko ya Gesi 3,255 Kutolewa Kwa Bei ya Ruzuku Longido

📌Wananchi wamshukuru Rais Samia  Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza usambazaji wa majiko ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku Wilayani Longido Mkoani Arusha ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034. Hayo yameelezwa Desemba 3, 2024 Wilayani Longido na Mhandisi wa Miradi wa REA, Kelvin Tarimo wakati wa mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Longido na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa wa kuelezea utekelezwaji wa miradi mbalimbali ya Serikali wilayani humo. "Tupo hapa Wilayani Longido kwa ajili ya kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni pamoja na kuanza rasmi uratibu wa mradi wa kusambaza na kuuza majiko ya gesi (LPG) ya kilo 6 ambapo kwa Wilaya ya Longido pekee jumla ya majiko 3,255 yatauzwa kwa bei ya ruzuku ya asilimia 50," amesema Mhandisi Tarimo. Mhandisi Tarimo amesema Wakala wa Nishati Vijijini unalo jukumu la kuhakikisha Watanzania wanaachana na matumizi ya nishati isiy...

Millioni 390 Kusambaza Majiko ya Gesi 19,350 kwa Bei ya Ruzuku Mkoani Mara

*📌Kila Wilaya kupata majiko 3,255* *📌RC Mara ahamasisha wananchi kuchangamkia fursa* Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kusambaza majiko ya gesi (LPG) ya kilo 6 yapatayo 19,530 Mkoani Mara ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034. Hayo yamebainishwa Desemba 2,2024 na Mhandisi Mwandamizi wa Wakala wa Nishati Vijijini(REA),Deusdedith Malulu ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi. "REA ni mdau mkubwa wa kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kwa awamu hii tumekuja na mradi huu wa majiko ya gesi," amesema Mha. Malulu. Amesema kwa awamu hii REA itasambaza jumla ya majiko ya gesi ya kilo sita 452,000 nchi nzima kwa gharama ya shilingi bilioni 8.6. Aidha, Mha. Malulu alizungumzia miradi mbalimbali inayoratibiwa na wakala ikiwemo uuzwaji wa sola za majumbani kwa bei ya ruzuku ya hadi 75% pamoja na uwezeshwaji wa ujenzi wa vituo vya bidhaa za mafuta ...

Mkutano wa Kikanda wa Matumizi Bora ya Nishati Waanza Kwa Mafaniko Arusha

Na Mwandishi Wetu Mkutano wa Kikanda wa Matumizi Bora ya Nishati unaojumuisha Viongozi na Wadau mbalimbali kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)  na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umeanza kwa mafanikio ambapo katika Siku ya kwanza Wadau wameweza kuonesha teknolojia mbalimbali za matumizi bora ya nishati ikiwemo majiko na magari. Katika Siku ya kwanza ya Mkutano, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amekagua mabanda ya Maonesho ya Wadau mbalimbali wanaoshiriki katika Mkutano huo ulioanza jijini Arusha ambao utafunguliwa rasmi kesho na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko. Pamoja na kukagua mabanda hayo ya maonesho, Dkt. Mataragio alikagua shughuli nyingine zinazoendelea kukamilishwa kuelekea siku ya ufunguzi rasmi wa Mkutano huo. Katika Mabanda ya Maonesho, Dkt. Mataragio alijionea vifaa mbalimbali vinavyotumia umeme kidogo ikiwemo majiko, Brenda, mashine za kusukuma maji na magari ya umeme. Dkt.Mataragio ame...

Mhe. Silaa Aagiza Kujengwa Mnara wa Mawasiliano Katika Kijiji Cha Msolokelo Morogoro

Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Morogoro. Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa (Mb) ametoa maelekezo kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kushirikiana na watoa huduma kujenga mnara wa mawasiliano katika kijiji cha Msolokelo, mkoani Morogoro ili kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma za mawasiliano ya simu na intaneti katika kijiji hicho. Waziri Silaa ametoa maagizo hayo leo Disemba 3, 2024 wakati wa ziara yake mkoani humo ya kukagua hali ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yenye changamoto sambamba na kukagua ujenzi wa minara inayojengwa mkoani katika mkoa huo ikiwa ni sehemu ya ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano inayoendelea kujengwa kote nchini. Waziri Silaa amewahakikishia wananchi wa Msolokelo kufikishiwa huduma za mawasiliano katika kipindi kifupi kijacho kwa kuwa Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan iko makini kuhakikisha kuwa vijiji vyote nchini vinapata huduma za mawasiliano kabla ya mwaka 2025 kumalizika. ...

Waziri Dkt.Pindi Chana apokea rasmi Tuzo ya Dunia

Siku chache baada ya Tanzania kutwaa Tuzo ya Dunia kuwa Sehemu Maridhawa Zaidi kwa Utalii wa Safari Duniani (World’s Leading Safari Destination 2024), Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana amepokea tuzo hiyo rasmi jijini Dodoma. Waziri Pindi Chana amepokea Tuzo hiyo mbele ya wadau wa utalii na uhifadhi wakiwemo maafisa wanyamapori kutoka wizara 138 nchini wanaohudhuria mafunzo mbalimbali ya utalii na uhifadhi mjini Dodoma na kusema Tuzo hiyo ni matokeo ya kazi kubwa ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na wadau wenyewe wa uhifadhi na utalii.

Serikali yasema Unyanyasaji dhidi ya Wenye Ulemavu Sasa basi

*📌 Dkt. Biteko asema Serikali itakula Sahani moja na wanyanyasaji wa wenye ulemavu* *📌 Wakuu wa Mikoa waagizwa kusimamia mpango wa taifa haki na Ustawi kwa wenye ulemavu* *📌 Halmashauri zatakiwa kutenga Bajenti ununuzi wa teknolojia saidizi kwa wenye ulemavu*   *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali haipendi kusikia na haitavumilia kusikia uwepo wa vitendo vya unyanyasaji kwa watu wenye ulemavu na wale watakaojihusisha na vitendo hivyo itawachukulia hatua kikamilifu. DKt. Biteko amesema hayo Jijini Dar es Salaam wakati akimwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa katika maadhimisho ya Siku ya watu wenye ulemavu iliyofanyika sambamba na uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Haki na Ustawi wa Watu wenye Ualbino na Mkakati wa Taifa wa Teknolojia Saidizi kwa wenye ulemavu. “Hatuwezi kuvumilia kuona watu wanaojihusisha na vitendo vya unyanyasaji wa watu wenye ulemavu, eti wananauza viungo vy...