Skip to main content

Posts

Showing posts from December 3, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TADB Yafanya Semina Elekezi kwa Wanahabari Kanda ya Ziwa-Mwanza

  Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo imeendesha semina elekezi kwa waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa, ikiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano, kuongeza uelewa kuhusu majukumu ya benki, na kuonesha mchango wake katika kuendeleza minyororo ya thamani ya kilimo nchini. Semina hiyo imefunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Saidi Mtanda, ambaye amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za kifedha na vyombo vya habari katika kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo. Kupitia ufadhili wa miradi ya kimkakati, TADB inaendelea kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo kwa kusaidia uzalishaji wa mazao ya kibiashara, ufugaji wa kisasa, uvuvi na uchakataji wa mazao ya samaki. Benki pia inaweka mkazo katika kuwawezesha vijana na wanawake kushiriki kikamilifu katika kilimo-biashara. Hadi sasa, zaidi ya Shilingi bilioni 631 zimetolewa kufadhili miradi 151 katika Kanda ya Ziwa. Kati ya hizo, Mkoa wa Mwanza umepokea jumla ya Shilingi bilioni 79.14 kwa ajili ya ...

Vijana Wabunifu Ndiyo Wenye Hatma ya Tanzania - Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Watanzania wanataka kuiona nchi yao ikifikisha lengo la uchumi wa kati wa dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050 na watakaofanikisha jambo hilo ni sekta binafsi ikiwemo wenye wabunifu kutoka kwenye kampuni changa. “Mtakumbuka kuwa Julai, mwaka huu Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alizindua DIRA 2050. Dira hii si ya Serikali peke yake bali ni kielelezo cha matarajio ya Watanzania ambao wanataka nchi yao ifikie uchumi wa kati wa dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050. Injini ya kuendesha nchi kuelekea maono haya ni sekta binafsi zikiwemo kampuni changa zinazoanzishwa,” amesema. Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Desemba 03, 2025) wakati akifunga maadhimisho ya Wiki ya Kampuni Changa za Teknolojia (start-ups) kwenye ukumbi wa PSSSF, Makumbusho, jijini Dar es Salaam. Waziri Mkuu ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kazi ya kufikisha lengo siyo ndogo na inahitaji mabadiliko ya kiu...

Makamu wa Rais Afungua Maadhimisho ya Wiki Ya Kimataifa ya Usugu wa Vimelea Vya Magonjwa Dhidi ya Dawa

*ASISITIZA USHIRIKIANO WA KIKANDA KUKABILIANA NA HALI HIYO* *ATOA WITO WA ELIMU KUENDELEA KUTOLEWA KWA WANANCHI JUU YA MATUMIZI SAHIHI YA DAWA* Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Tanzania imedhamiria kuhakikisha inalinda afya, maisha ya watu na mazingira kwa kutoa kipaumbele katika uimarishaji wa mfumo wa afya, kuwekeza katika utafiti wa kisayansi, na kuhimiza matumizi ya dawa kama yanavyokusudiwa kwa manufaa ya watanzania na dunia kwa ujumla.   Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Maadhimisho ya Kanda ya Afrika ya Wiki ya Kimataifa ya Usugu wa Vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa, yanayofanyika Hyatt Regency, Jijini Dar es Salaam. Amesema hatua hizo ni katika kukabiliana na tishio linaloongezeka la usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, ambapo pia ametoa wito kwa nchi za Afrika kujiunga katika mapambano hayo ya kimataifa kwa kuunga mkono juhudi za matumizi sahihi ya dawa hizo za kuokoa maisha, kwa kubadilishana uj...