Skip to main content

Posts

Showing posts from July 21, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WIZARA YA MALIASILI NA TAASISI ZAKE ZAJIPANGA UJIO WA MAONESHO YA NANENANE

 ðŸ“ŒKamati ya kitaifa yakutana kwa ajili ya maandalizi na kutoa mwelekeo wa ushirikiano wa Wizara 📌Maliasili yajipanga kuleta wanyama hai na kutangaza vivutio vya Utalii Dodoma  📌Taasisi zajipanga kutoa huduma bora kwa wananchi Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma KAMATI ya kitaifa ya Kuratibu maandalizi ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) kwa Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake imekutana leo Julai 21,2026 Jijini Dodoma na kuazimia kutoa huduma bora kwa wananchi ili watambue kazi na majukumu ya Wizara na taasisi zake. Akizungumza na kutoa maelekezo ya namna ya kuboresha ushiriki wa Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake kwenye maonesho ya nanenane, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii, Richard Wandwi amesema, ushiriki wa Wizara kwa mwaka huu unapaswa kuwa wa kiubunifu na kutangaza maeneo ya vivutio vya utalii kwa Mkoa wa Dodoma kama ilivyoainishwa kwenye mkakati wa uendelezaji utalii kwa mkoa wa Dodoma uliozinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe Dkt Mwigulu Nchemba. ‘’ Naomb...

RAIS SAMIA AONDOKA NCHINI KUELEKEA NCHINI GHANA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiondoka nchini kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Julai, 2026 kuelekea Accra, Ghana ambapo atashiriki katika Mkutano Mkuu Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu afya, utakaofanyika tarehe 22 Julai, 2026 jijini Accra.

MAPINDUZI YA UMWAGILIAJI: SERIKALI YASAMBAZA PAMPU 2,000, YACHIMBA VISIMA 390 KUINUA KILIMO

Njedengwa, Dodoma Serikali imeongeza kasi ya mapinduzi ya sekta ya kilimo kwa kuanza kusambaza pampu za umwagiliaji na kuchimba visima 390 katika mikoa 15, hatua inayolenga kuwawezesha wakulima kulima mwaka mzima, kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha usalama wa chakula nchini. Mpango huo unatarajiwa kunufaisha wakulima 15,022 waliounganishwa katika vikundi 769, huku ekari 13,518.75 zikiingizwa kwenye kilimo cha umwagiliaji ili kupunguza utegemezi wa mvua. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa, alisema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuwainua wakulima wadogo, hususan wanawake na vijana, kwa kuwapatia uhakika wa maji kwa ajili ya uzalishaji. Alisema pamoja na kuendelea na ujenzi wa miradi mikubwa na ya kimkakati ya umwagiliaji, Serikali imeamua kuwekeza pia katika uchimbaji wa visima na usambazaji wa pampu kwa vikundi vya wakulima ili kuongeza tija mashambani. "Tumeelekezwa kutaf...