Mwenyekiti wa Chama Chamapinduzi(CCM)Rais Samia Suluhu Hassan amewasilisha katika Mkutano Mkuu wa CCM Jina la Mwanasiasa Mkongwe nchini Steven Wasira kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara. Wasira anatarajia kumrithi Abdulrahman Kinana aliyeomba kupumzika nafasi hiyo mwezi Julai Mwaka Jana. Kupitia mkutano huo mkuu maalum wa CCM,Wajumbe 1924 wa mkutano huo wanatarajia kupiga kura za ndio au Hapana ili kupitisha Jina hilo la Wasira.
Marato tv - Sauti ya Jamii