Katika kuendeleza Ushirikiano kati ya Tanzania,Zambia na China ulioanzishwa na Viongozi wa nchi hizo akiwemo Rais wa Awamu ya Kwanza na Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,Kenneth David Kaunda wa Zambia na Rais wa Awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Watu wa China,Mao Ze Dong,serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imeingia makubaliano na China ili kuweza kujenga na kuiboresha Reli ya TAZARA iliyojengwa kutoka mwaka 1970 hadi 1975. Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Patrobas Katambi wakati wa Kumbukumbu ya Kuwakumbuka Wataalamu 65 wa Kichina walioshiriki Ujenzi wa Reli ya TAZARA. Akizungumza katika eneo la makaburi lililopo katika eneo la Gongolamboto Jeshini,jijini Dar es Salaam,Waziri Katambi amesema msingi wa ushirikiano ulioanzishwa na waasisi wa nchi hizo katika Nyanja ya Uchumi,Siasa,Teknolojia na Utamaduni imeendelezwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo watanzania wameshuhudia miradi mbalimbali iliyojen...
Marato tv - Sauti ya Jamii