Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ameizindua Shule ya Msingi Kasoma iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, mkoani Mara na kuipongeza halmashauri hiyo kwa kusimamia miradi ya maendeleo kwa kuzingatia thamani ya fedha pamoja na kuendelea kuboresha huduma za elimu kwa wananchi. Akizungumza baada ya kuzindua shule hiyo leo (Jumamosi, Julai 4, 2026), Dkt. Mwigulu alisema Serikali itaendelea kuwekeza katika sekta ya elimu ili kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata fursa ya kusoma katika mazingira bora na karibu na makazi yao. "Nimeona usimamizi mzuri wa miradi unaozingatia thamani ya fedha. Hicho ndicho ambacho Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amekikusudia kiwafikie wananchi. Hongereni sana," alisema Dkt. Mwigulu. Waziri Mkuu alisema Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imeanza mapema kutekeleza mwelekeo wa Serikali wa kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na shule ya sekondari, hatua ambayo itawezesha utekelezaji wa sera ya elimu ya lazima kwa miaka 10 kuanzia shule ya msingi ha...
Marato tv - Sauti ya Jamii