Skip to main content

Posts

Showing posts from April 14, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TRC imepata Mafanikio Makubwa Kwa Kusafirisha Abiria ya Milioni 5.5 Kwa Treni ya SGR

 Shirika la Reli Tanzania (TRC) lilianza kutoa huduma ya usafirishaji abiria kutumia reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) mnamo mwezi Juni 2024, toka kipindi hicho mpaka Machi 2026, abiria 5,512,995, wamesafiri kwa kutumia treni za SGR.   Takwimu hiyo ina ujumbe mkubwa sana kimkakati kuhusu ubora na mafanikio ya huduma ya SGR, na ina maana zifuatazo: Kwanza ni Kukubalika kwa Huduma (High public acceptance) Abiria zaidi ya milioni 5.5 ndani ya muda mfupi inaonyesha kuwa, Wananchi wameikubali kwa kiwango cha juu kabisa, huduma ya SGR kwani mejenga imani kubwa kwa watumiaji. Ukiachana na hilo, SGR imekuwa chaguo kuu la usafiri ukilinganisha na njia nyingine na usafiri na usafirishaji, lakini kubwq zaidi hii ni ishara ya market penetration yenye mafanikio makubwa. Pili inadhihirisha Ufanisi wa Utoaji Huduma (Service Efficiency), na kwa muktadha huo, idadi hii inaashiria kuwa, huduma inapatikana kwa uhakika na ratiba zinazingatiwa , katika kipindi chote hicho uendeshaji umekuw...

Jaji Mkuu Akutana na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi

Dodoma Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju, leo tarehe 14 Aprili, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera, kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Dkt Tulia Afanya Mazungumzo Ujumbe wa Tanzania Katika Umoja wa Mabunge Duniani Nchini Uturuki

 Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 152 wa Umoja wa Mabunge Duniani unaoogozwa na Mheshimiwa Naibu Spika wa Bunge Mhe. Daniel Sillo (Mb) umekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa IPU na Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) katika Hoteli ya Hilton Istanbul Bomonti Jijini Istanbul, Uturuki. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Sillo amewasilisha salamu za Spika wa Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) na kutambulisha Ujumbe wa Tanzania ulio pamoja nae kushiriki Mkutano huo unaotarajiwa kuanza rasmi tarehe 15 hadi 19 Aprili 2025, jijini humo.  Mhe Silo alieleza utayari wa Tanzania katika kuitangaza Tanzania kupitia fursa na vivutio vyake pamoja na kuwakaribisha Wajumbe wa Umoja wa Mabunge, kushiriki Mkutano wa 153 ambao Tanzania atakuwa Mwenyeji.  Aidha, utayari wa Wajumbe wapya wa Uwakilishi wa Tanzania katika kuhakikisha wanapata nafasi mnalimbali za uwakilishi ndani ya Umoja na kuendelea kuitekeleza sera ya diplomasia ya kibunge na kiuchumi. Waheshimiwa Wabunge wa...

Bunge Marathon 2026 Mbio za Kihistoria-Sanga

MWENYEKITI wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, amesema mashindano ya Bunge Marathon 2026 yanatarajiwa kuwa ya kipekee mwaka huu, yakilenga kuvunja rekodi na kuibua ushindani wa hali ya juu zaidi nchini. Ameeleza kuwa tukio hilo litafanyika rasmi tarehe 18 Mei 2026, likiwa limeboreshwa kwa kiwango kikubwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa itakayorahisisha usimamizi wa mbio na kuhakikisha matokeo yanakuwa sahihi na ya kuaminika. Sanga amesisitiza kuwa moja ya mambo yanayovutia zaidi ni ushiriki wa wazi kwa kila mtu, akibainisha kuwa mashindano hayo hayana mipaka ya uzoefu,hivyo kuwapa nafasi wanariadha wa kitaalamu na wananchi wa kawaida kushiriki na kuonesha uwezo wao. Ameongeza kuwa matarajio ni kuona idadi kubwa ya washiriki ikiongezeka mwaka huu, huku Bunge Marathon 2026 ikilenga kuweka historia mpya na kuendelea kuhamasisha afya, mshikamano na ari ya ushindani miongoni mwa Watanzania. "Maandalizi ya mbio za Marathon ya Wabunge yanayoandaliwa kwa mara ya kwanza yamekamilika, huku tuki...

Taifa Gasi yaunga mkono jitihada za serikali matumizi ya Nishati safi

  Na MASHAKA MHANDO, Lushoto IMEELEZWA kuwa zaidi ya Watanzania 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya nishati zisizo safi kama kuni na mkaa, hali inayolifanya Taifa kuingia katika msiba mzito wa nguvu kazi kila kukicha. Kufuatia takwimu hizo za kutisha, Kampuni ya Taifa Gas, ambayo ni kinara wa nishati safi nchini, imetangaza kuongeza uwekezaji wake na kasi ya usambazaji wa gesi ili kuunga mkono juhudi za dhati za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anayepigania matumizi ya nishati mbadala barani Afrika na duniani kote. Akizungumza Leo wilayani Lushoto, Meneja wa Masoko wa Taifa Gas, Oscar Shelukindo, amebainisha kuwa kampuni hiyo sasa inashikilia asilimia 51 ya soko la gesi nchini, ikiwa ni matokeo ya uwekezaji mkubwa katika miundombinu inayolenga kumkomoa mwanamke wa Kitanzania na mazingira kwa ujumla. "Mafanikio haya ya kumiliki asilimia 51 ya soko yametokana na dhamira yetu ya kuunga mkono juh...

Daktari wa Shifaa afichua vijana wanavyokufa ghafla na shinikizo la damu

Daktari bingwa wa maradhi ya moyo wa hospitali ya Shifaa iliyoko Msese Kinondoni jijini Dar es Salaam, Lulu Mageta amewataka vijana kupima afya zao mara kwa mara kwani wengi kwa sasa wanakabiliwa na maradhi ya shinikizo la damu. Amesema zamani ilionekana kuwa watu wazima ndio wako kwenye hatari ya kupata maradhi ya shinikizo la damu lakini kwa sasa vijana  wengi chini ya miaka 40 wanasumbuliwa na tatizo hilo. Dk Lulu aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia ongezeko la magonjwa ya moyo hasa kwa vijana waliochini ya miaka 40 na punguzo lililotolewa na hospitali hiyo kwa vijana wanaotaka kuchunguzwa afya ya moyo. Alisema vijana nao wanatakiwa kujenga utamaduni wa kupima afya ya moyo mara kwa mara kujua afya zao badala ya kusubiri mpaka hali inapokuwa mbaya ndipo waende hospitali. “Zamani ilionekana kuwa maradhi ya shinikizo la damu yanawashambulia watu wazima sana pekee lakini kutokana na kubadilika kwa mtindo wa maisha watu wengi hawafanyi mazoezi kwa hiyo vijana...

Wananchi Nyakabale Geita Wamwomba Waziri Mkuu Aingilie Mgogoro kati yao na Mgodi wa GGM

Na Mwandishi Wetu Wananchi wa eneo la bondeni katika Kijiji cha Nyakabale mkoani Geita, wanamuomba Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Lameck Nchemba aingilie kati mgogoro unaoendelea kati yao na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) kuhusu mpango wa uhamishaji na fidia. Wananchi hao wameyasema hayo leo baada ya Mgodi huo mkubwa kabisa Tanzania na Afrika kutamka mbele ya Hashim Komba ambaye ndiye Mkuu wa Wilaya ya Geita kwamba hawana mpango wa kuwalipa wananchi Zaidi ya 135 wanaoishi katika maeneo hayo mkoani Geita. Awali, katika taarifa iliyowasilishwa kutoka katika Kamati Maalumu ambayo iliundwa na Mkuu wa Wilaya kushughulikia mgogoro huo ambayo taarifa yake amekabidhiwa DC huyo ilisema kwamba GGM hawana nyaraka zozote ambazo zinaonyesha kuwa wameshalipa wananchi wanaoishi katika eneo hilo. “Hakuna documents zozote ambazo zinaonyesha kuwa eneo hilo limeshalipwa na Mgodi wa GGM. Tumewafuata mara kadhaa watupatie documents lakini hakuna,” taarifa iliyowakilishwa kwa DC alisema hivyo. Kwa upande wake Afi...

Geita's Nyakabale Land Dispute Escalates as Residents Threaten to Block Mine Access Road

  By Staff Writer Tensions between Geita Gold Mine (GGM) and residents of Nyakabale’s lowland have escalated after villagers threatened to block the road leading to the mine in protest over unpaid compensation, prompting the Geita District Commissioner to intervene and call for calm. The threat came during a heated meeting today where GGM, Tanzania’s largest gold mine and one of Africa’s biggest, told Geita District Commissioner Hashim Komba that it has no plans to compensate more than 135 residents living in the area. The declaration sparked outrage among villagers who say they will not vacate their land without payment. Earlier, a special committee formed by Komba to investigate the dispute submitted a report stating that GGM has no documentation proving the residents have already been compensated. “There are no documents at all showing that the area has been paid for by GGM. We have repeatedly asked them to provide the documents but there is none,” the report presented to the DC...

Dkt.Mwigulu: Tunatambua mchango wa wafanyakazi

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wafanyakazi wa sekta ya umma na sekta binafsi katika kukuza uchumi na maendeleo ya Taifa. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu ameyasema hayo jana jioni Aprili 13, 2026 jijini Dodoma katika Hafla ya Maandalizi ya Mei Mosi, 2026 ambayo Kitaifa inafanyika mkoani Njombe. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema Serikali inaendelea kuwaenzi wafanyakazi nchini kutokana na umuhimu wao mkubwa kwa Taifa. Katika hafla hiyo ya awali, kiashi cha shilingi bilioni 1.105 kimekusanywa ambapo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu alisema fedha hizo zitausaidia mkoa mwenyeji kukamilisha shughuli za maandalizi kwa ajili ya tukio hilo. Mheshimiwa Waziri Mkuu aliongeza kwa kulipongeza Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) kwa ubunifu wa kuhakikisha maadhimisho ya Mei Mosi yanaacha alama katika mkoa mwenyeji. “Wenzetu TUCTA wamekuja na ubunifu kwamba shughuli za Mei Mosi zinaacha alama katika mkoa husika kwa kutekeleza miradi mbalimbali kama wa...