Skip to main content

Posts

Showing posts from August 13, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Katavi Wampa Heko Rais Samia Umeme Vijijini

*📌Fursa lukuki za kiuchumi zaibuliwa* *📌Wananchi waeleza namna maisha yao yalivyobadilika* Wananchi wa Kijiji cha Mapili Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadili maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Wametoa shukrani hizo kwa nyakati tofauti kijijini hapo Agosti 13, 2025 wakati wa kampeni maalum ya uhamasishaji wa matumizi ya umeme kwa ajili ya shughuli za kiuchumi inayotekelezwa na REA katika maeneo mbalimbali kote nchini. “Tunaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kabla ya kupata nishati hii ya umeme mazingira hayakuwa mazuri, usiku hatukuwa na mwanga sasa hivi tunaishi kwa amani na hata baadhi ya shughuli za kimaendeleo zinafanyika hadi muda wa usiku lakini pia tunapata habari kwa kutazama luninga muda wowote tunaotaka pia baadhi ya vijana wamepata ajira kupitia umeme,” alisema Mwalimu Mstaafu, Mkazi wa Ki...

Waziri Mkuu Akagua Mabasi Miundombinu ya Mradi wa BRT Awami ya pili

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 13, 2025 amekagua mabasi mapya kwa ajili ya awamu ya pili mradi wa mabasi yaendayo haraka (BRT-2) pamoja na miundombinu ikiwemo kituo kikuu cha mabasi hayo cha Mbagala Rangi tatu na kituo cha gerezani, jijini Dar es Salaam. Katika ukaguzi huo, Mheshimiwa Majaliwa ametembelea ujenzi wa kituo maalum cha kujazia gesi kwa ajili ya mabasi hayo, kinachojengwa katika kituo cha Mbagala Rangi Tatu. Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Waziri Mkuu amewaagiza waendeshaji wa mradi huo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha maeneo yaliyobaki yatakayowezesha mradi huo kuanza kutoa huduma ndani ya mwezi huu. Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu aliambana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) William Lukuvi, Naibu Waziri Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Zainab Katimba, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi pamoja na watendaji wengine wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Wakala ya Mabas...

Tanzania Yajipanga Kuwa Kitovu Cha Utengenezaji wa Bidhaa wa Huduma Migodini Kusini Mwa Jangwa la Sahara

▪️Waziri Mavunde azindua Ghala la Mauzo ya vipuri vya Mitambo na Mashine kubwa za Madini ▪️Ni uwekezaji wa Kampuni kubwa za Mitambo kutoka India na Italia ▪️Vipuri vya mitambo na mashine kubwa za uchimbaji kupatikana nchini ▪️Rais Samia apongezwa kwa mazingira mazuri ya uwekezaji Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amesema Tanzania inajipanga kuwa kitovu cha utengenezaji wa bidhaa na huduma migodini kwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara kwa kuvutia uwekezaji kwenye viwanda vya kutengeneza bidhaa za migodini na utoaji wa huduma kwenye migodi ya ndani na nje ya nchi. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati akizindua ghala la mauzo ya vipuri vya mitambo mikubwa  na vifaa  vya uchimbaji madini ambalo linamilikiwa kwa ushirikiano kati ya Kampuni ya Shan Parts Africa ya India na Kampuni ya ITR  ya Italy. “ Nawapongeza sana Kampuni ya Shan Parts na ITR kwa uamuzi wa kuwekeza nchini Tanzania kwenye vipuri vya mitambo mikubwa na vifaa vya uchimbaji madini....

Sadc na Marekani Kuanzisha Jukwaa la Majadiliano

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki kikao cha awali cha maafisa waandamizi cha Jukwaa la Majadiliano kati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Serikali ya Marekani kilichofanyika Antananarivo, Madagascar Agosti 13, 2025. Akitoa neno la ufunguzi wa majadiliano hayo, Naibu Katibu Mtendaji wa SADC anayeshughulikia ushirikiano wa Kikanda, Bi. Angeles N'Tumba alisema kikao hicho ambacho ni cha kwanza kufanyika, kitajadili miongozo ambayo SADC na Marekani wataitumia katika ushirikiano wao ambao umelenga maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na amani na usalama, afya, uchumi na usimamizi wa rasilimali kama vile nishati na madini. Mwakilishi wa Serikali ya Marekani ambaye ni Naibu Katibu Mkuu anayeshugulikia masuala ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Melanie H. Higgins ameihakikishia SADC kuwa licha ya  mabadiliko ya Sera katika Serikali ya Marekani, nchi hiyo ...