*📌 Ahoji matumizi ya Shilingi milioni 159 nje ya bajeti Ujenzi wa Kituo cha Afya Msimbati* *📌 Mkurugenzi wa Halmashauri na Wataamu watofautiana Majibu* *📌 Aiagiza TAKUKURU Kufanya Uchunguzi Ujenzi wa Kituo cha Afya* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Novemba 17, 2024 amefanya ziara Wilayani Mtwara na kukagua ujenzi wa miradi inayotekelezwa kwa fedha zinazotolewa na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya kuboresha maendeleo kama njia ya kurejesha rasilimali kwa wananchi kupitia (CSR). Akikagua Kiktuo cha Afya Msimbati, Dkt. Biteko ameeleza kutoridhishwa na matumizi ya fedha iliyokuwa imepangwa kutumika katika ujenzi wa kituo hicho na kupelekea ongezeko la kiasi cha shilingi milioni 159. Kituo hicho cha Afya awali kilikadiriwa kujengwa kwa gharama ya shilingi milioni 600 lakini gharama za ujenzi huo ziliongezeka hadi kufikia shilingi milioni 759 na hivyo kuibua maswali ambayo Mkurugenzi wa Hal...
Marato tv - Sauti ya Jamii