POLISI katika Kaunti ya Kilifi Nchini Kenya wanachunguza iwapo kundi la imani potovu lililonaswa mwanzoni mwa Wiki katika eneo la Binzaro, lina uhusiano na dhehebu la Shakahola ambalo lilisababisha vifo vya zaidi ya watu 400. Boma ambalo mwanamume alipatikana amefariki na watu wengine wanne wakiwa katika hali dhaifu Jumatatu, liko karibu kilomita saba kutoka barabara kuu ya Malindi–Sala Gate. Ndani ya boma hilo kuna nyumba tatu zilizojengwa kwa udongo na paa za mabati lakini hazina madirisha yoyote. Kuna bwawa la maji ambalo halijakamilika kujengwa, banda la kuku, na eneo la kupikia nje. Mahali hapo hakuna vitanda, jambo ambalo linaashiria kuwa wakazi walilala sakafuni. Choo kinachoonekana kama banda dogo kilichofichwa katika vichaka karibu na lango kuu, kuashiria mazingira magumu kwa wakazi. Sehemu mbalimbali za ardhi zilikuwa zimevurugwa na hivyo kuibua hofu ya kuwepo kwa makaburi, jambo ambalo maafisa wa polisi sasa wanajaribu kuthibitisha. Wapelelezi walimkamata mshukiwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii