Skip to main content

Posts

Showing posts from February 28, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt Tulia Amwaga Bima za Afya Kwa Maelfu ya Wananchi Jijini Mbeya

Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge Jimbo la Mbeya Mjini Mhe.Dkt.Tulia Ackson amekabidhi Bima za Afya Kwa Wananchi takribani 9000. Hafla ya Makabidhiano ya Human hizo zap afya imefanyika katika Uwanja wa Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya na kuhuduriwa na viongozi mbalimbali ikiwemo kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mbeya Mh.Juma Zuberi Homera, Naibu Meya Mh.Kephafas, madiwani pamoja na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya Jiji la Mbeya. Akizungumza wakati wa kukabidhi Kadi za Bima ya afya kwa Walengwa,Dokta Tulia amesema uamuzi huo umelenga kuwezesha Wananchi kupata matibabu katika Vituo Vya Afya , zahanati na hospital bila kuwepo kwa kikwazo chochote cha fedha. 

Waziri Mkuu Ameomba Viongozi Wa Dini na Watanzania Wasichoke Kuunga Mkono Serikali ya Awamu ya Sita

 “Ninatoa rai kwa viongozi wa dini na Watanzania wote msichoke kuiunga mkono serikali yenu, ili sote tuendelee kuishi pamoja kwa amani, upendo na mshikamano. Serikali inatambua wajibu mkubwa wa kiroho mlionao ambao unaleta matokeo chanya katika maisha yetu ya kila siku, endeleeni kujitoa kwa ajili ya Taifa letu, viongozi na wananchi wake, hatuna mashaka na imani yenu na mapenzi yenu kwa serikali-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Mijadala Mikubwa ya Kuboresha Ufundishaji na Ujifunzaji wa Elimu Kufanyika Musoma Vijijini

Na Shomari Binda-Musoma Kongamano kubwa la mijadala ya uboreshaji na ufundishaji kujenga uelewa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari litafanyika kwa siku 3 jimbo la Musoma vijijini. Wataalamu wa elimu watakaoongoza kongamano hilo litakalofanyika machi 25 hadi 27 jimboni humo ni Dr. Zablon Kengera kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),Dr. George Kaangwa, UDSM na Jeff Makongo mtaalam wa ubunifu (Ubunifu Associates) Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo februari 28/2025,Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof.Sospeter Muhongo atagharamia kongamano hilo kwa siku hizo tatu.  Taarifa hiyo imedai mjadala wa kwanza utafanyika machi 25 Mwaka huu kwenye shule ya sekondari ya Busambara ambapo washiriki watakuwa maafisa elimu Kata 21 wataalam na wadau wengine wa elimu Mjadala wa pili utafanyika machi 26 kwenye shule ya msingi Busambara  kuanzia saa tatu za asubuhi hadi Saa sita za mchana hyku washiriki wakiwa walimu wakuu 120 na wataalamu watatu na baadaye kuanzia saa nane m...

Mariam Mwinyi Azindua Kampeni Ya #weareequal Ya Oaflad Tanzania.

Mke wa Rais wa Zanzibar,  Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) , Mhe.Mama Mariam Mwinyi amesema takriban wananchi 5,000 wamepatiwa huduma za afya jumuishi kwa watu wa makundi yote hususan Wanawake, Watoto,  Vijana na Watu wenye ulemavu kupitia kambi za matibabu za Afya Bora, Maisha Bora chini ya ZMBF. Mariam Mwinyi amesema hayo alipozindua Kampeni ya "We Are Equal" (yaani kwa Kiswahili Tupo Sawa) inayoratibiwa na Taasisi ya  Maendeleo ya Wake wa Marais wa Afrika (OAFLAD) na kufunga kambi ya nne ya matibabu ya "Afya Bora, Maisha Bora" katika Viwanja vya Hospitali ya Kitogani,  Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 28 Februari, 2025. Aidha , Mariam Mwinyi ameeleza kuwa Tanzania inakuwa nchi ya 22 kuzindua Kampeni hii kati ya nchi 54. Ambayo ndio nchi ya mwisho kuzindua katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa kampeni hii.  Halikadhalika,  Mariam Mwinyi amesema Kambi ya Matibabu inaunga mkono juhudi zinazofanywa na Serika...

Mara yaliomba Shirika la Emedo Kupanua Shughuli zake

Na Rs; Mara Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Dominicus Lusasi Februari 28 Mwaka huu amezindua Mpango Shirikishi wa Uvuvi Salama katika Kijiji cha Busekela, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.  Mpango huo unatekelezwa na Shirika lisilo la kiserikali la EMEDO ambalo Lusasi ameliomba shirika hilo kupeleka elimu ya kuzuia kuzama maji katika Wilaya nyingine za Mkoa wa Mara zinazozunguka ziwa Victoria.  Lusasi amesema ajali za majini zimesababisha watu wengi kupoteza maisha na kuwa chanzo cha familia nyingi kuishi maisha duni kwa kupoteza nguzo muhimu katika familia zao.  “Eneo kubwa la Mkoa wa Mara linazungukwa na Ziwa Victoria na mradi huu unavisaidia vijiji viwili tu vya Wilaya ya Musoma, kama itawezekana tunaomba mpanue huduma za mradi huu ili Wilaya zote zinufaike na mradi huu” amesema Bwana Lusasi.  Lusasi amesema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka watu laki tatu duniani hupoteza maisha kwa kuzama maji na zaidi ya asilimia 90 ya vifo hivyo vinatokea katika nchi...